Dortmund wamsajiri Karim Adeyemi

Klabu ya Borussia Dortmund wamemsajiri mshambuliaji wa kimataifa wa Ujerumani Karim Adeyemi kutoka nchini Australia kwenye klabu ya Salzburg ambao ni mabingwa wa nchi hiyo leo jumanne.

Klabu ya Dortmund imesema kijana huyo mwenye miaka 20 amesaini mkataba na klabu hiyo ambao utamuweka hadi june 2027 baada ya kumaliza vipimo vya afya leo mapema.

“Adeyemi ni mchezaji mwenye kipaji cha hali ya juu, mshambuliaji huyo kijana wa kijerumani ambaye ni nzuri kwenye nafasi ya umaliziaji na atasaidi kuongeza thamani ya aina ya ushambuliaji wetu,” mkurugenzi wa michezo Michael Zorc alisema.

Baada ya uusajiri wa  Niklas Süle na Nico Schlotterbeck, tunapata mchezaji mwingine anayevutia msimu ujao.

Sebastian Kehl, ambaye atamrithi Zorc msimu ujao, alisema kwamba Adeyemi alikuwa ni shabiki wa Dortmund katika maisha yake ya utotoni na kwamba ameamua kusaini kwenye klabu hiyo licha ya klabu kadhaa kubwa kutaka saini yake.

Adeyemi ameongoza kwenye ligi ya Australia kwa kufunga magoli 19, na ameifungia Salzburg magoli matatu kwenye ligi ya mabingwa. Pia amefanikiwa kuichezea Ujerumani kwenye kufuzu kombe la dunia dhidi ya Armenia.


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.