Klabu ya Liverpool leo imesitisha mazoezi ambayo yalipangwa kufanyika leo kutokana na kuongezeka kwa visa vya Uviko-19 kuelekea mchezo wa nusu fainali ya Carabao Cup
Mchezo wa Carabao Cup wa nusu fainali kati ya Liverpool na Arsenal upo kwenye hatari ya kuweza kuahirishwa kutokana kuongezeka visa vya Uviko-19 katika upande wa klabu ya Liverpool.

Inaeleweka kuwa majogoo wa Anfield walikuwa waanze mazoezi leo jioni, lakini yamehairisha huku mchezo wao ukiwa umepangwa kuchezwa siku ya tarehe ya 6/1/2022 alhamisi, mpaka muda huu hakuna taarifa yeyote ya kuahirishwa kwa mchezo huo japo klabu ya Liverpool wapo kwenye mazungumzo na EFL.
Ikiwa timu zote zitakuwa na wachezaji 14 wakiwemo makipa wawili, basi mchezo utaendelea kama kawaida, awali Majogoo iliwakosa wachezaji wake tisa wa kikosi cha kwanza kwenye mchezo dhidi ya Chelsea, huku pia wakiwapoteza wchezaji wake mahiri Mohamed Salah, Sadio Mane na Naby Keita ambao wamerudi Afrika kucheza AFCON.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


