Mwaka 2007 Tanzania iliishuhudia nafsi mpya inayokuja na dumu la petrol kwenye moto wa soka nchini. Alikuwa kijana mdogo tu wa miaka 19. Marcio Maximo alimuamini ugenini dhidi ya Burkina Faso. Na yeye hakumuangusha, aliifungia Tanzania bao la ushindi. Ni Erasto Edward Nyoni.

Ulikuwa mchezo wa kutafuta nafasi ya kufuzu michuano ya AFCON ya mwaka 2008 iliyokuwa ipigwe Ghana. Watanzania walikuwa hawamfahamu Nyoni ni nani. Nakumbuka hadi mtangazaji wa TVT siku ile Juma Nkamia alikosea, akasema mfungaji wa bao ni Haruna Moshi ‘Boban’ badala ya Erasto Nyoni. Kiukweli watanzania walikuwa hawamfahamu.
Kipindi hicho alikuwa anacheza Vitalo ya Burudani. Alikuwa ‘suprise package’ kwenye ukuta wa Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Salum Swedi, Amir Maftah na Shadrack Nsajigwa ‘Fuso’ aliyekula umeme dakika ya 62. Ulikuwa mchezo wa kwanza wa timu ya taifa kwa Nyoni ila alicheza kama ana uzoefu wa mechi mia moja.

Alianza maisha yake ya soka katika academy ya Rolling Stone chini mzee Ally Mtumwa pale mjini Arusha. Baadae kocha wa AFC-ARUSHA, Madaraka Bendera akavutiwa na uwezo wake. Akamsajili ajiunge na timu ya watoto ya AFC. Baadae alijiunga na Vitalo baada ya AFC kushuka daraja. Azam walimrudisha nyumbani mwaka 2010. Miaka saba baadae akajiunga na pori lilipo makutano ya Uhuru na Msimbazi.
Nakumbuka free-kick yake ya kusawazisha pale Sudan kabla ya Ditram Nchimbi kutupa bao la ushindi la kutupeleka CHAN.


mwakalosi
anakwenda na utamu wake nyoni mchezaji mwenye kipaji kikubwa kinachoisha ndani ya mipaka ya Tanzania
Hamidu
Kiraka mwenye uwezo wake , nyoni nakubali Sana..mchezaji tegemeo timu ya simba sc & taifastars#meridianbettz
Evaluziga
Nimchezaji mzuri ambae anastaili sifa
Amani
Nakumbuka free-kick yake ya kusawazisha pale Sudan kabla ya Ditram Nchimbi kutupa bao la ushindi la kutupeleka chan #meridianbettz
felister
ana uwezo mzurii tu
Mwanaidi
Nyoni yupo vizuri sana aisee ni vyema kuaminiwa
Isaya massawe
Kijana yuko vizuri Sana
Gabriel
Wa kawaida tu
David pere
Hii ni mashine kwelikweli anapokiwa uwanai Basi nyavu zake haziguswi
Rehema
Iko poa sana
Furahav
Yuko vizuri sana nyoni.
Ester jackson
Nyoni aliwafanya watanzania wote kunyanyuka na kuweka bendeza juu ilikuwa furaha sana
Salma
Yupo vizuri
Neema juma
Kijana mahiriii sana anastahili pongezi kwakee
Samiah
Nyoni yuko poa
Rehema Dickson
Nakumbuka free-kick yake ya kusawazisha pale Sudan kabla ya Ditram Nchimbi kutupa bao la ushindi
Shafii
Erasto Yuko vizuri Sana
Lydia Emmanuel Magoti
Erasto nyoni mshamburiaji mzuri anajua mpambanaji apingwi
Zeiyana
Nyoni mchezaji hanayejua majukumu yake hanatisha sana
Hope mwaikuka
Yuko poa tu mshikaj
Genia Sikaluzwe
Erasto nyoni ni wakawaida sana
Theckla
Nyoni yuko vizuri
Lombo
Erasto nyoni##@%Erasto mashine
dorophina
Nyoni yuko vizuri sana
aisha
Erasto namkubali sana
Antony Luseno
Aliaminika ni kweli akaonesha uwezo
mathayo sonje
nikikumbuka ile mechi ilikua ni ngumu sana, lakini kutokana na umakini wa erasto nyoni alibadilisha upepo baada ya kutupia goli ambalo lilimshangaza kila mmoja. #meridianbet
Ester mmakasa
Duuh!Erasto Nyoni yuko vizuri kwakweli ukilinganisha na umri wake bado unamruhusu kuendelea na makubwa kwenye soka ,akaze buti atafika mbali kama Samatta.
Frank Patrick
Nyoni fundi sana
Magdalena
Nyoni namkubali sana
Caroline
Erasto uyoooo
Kenani
Yuko vzr Sana hyu jamaa anajituma sana
Elika
Sifa zote nampa erasto nyoni..ni mchezaji mzur sana kwangu
Warda
Nyoni mnyama #Meridianbettz
Ernest
Erasto anauwezo mkubwa sana
Asia Abdy
Nyoni mtu hatari
Aziza mushi
Asanteni kwa habari meridian
Mwajuma
Ni namba 6 Mzuri sana hapa tanzania na anaitendea haki jezi ya timu yake
Sadick
Story ya kuvutia. Kwa sasa umri umemutupa mkono anakaribia kustaafu#meridianbettz
Mwanahamisi
Nyoni ni mtu hatari
Povel
Kiraka anayejuah majukum yake uwanjan
Emmy cleopa
Ahsante kwa habari