Majeraha Yanavyomkwamisha Straika Namungo

BENCHI la ufundi la Namungo limefunguka kuwa majeraha ya straika wao, Relliants Lusajo ndio yaliyomkwamisha kwa msimu huu kufanya vizuri kwenye ligi.

Lusajo kwa msimu huu amefanikiwa kufunga mabao 10 na kufanikiwa kutoa assisti sita. Pia amekuwa miongoni mwa wachezaji muhimu kwenye kikosi cha Namungo kwa msimu, magoli yake yameisaidia timu hiyo kumaliza nafasi ya tano kwa kujikusanyia alama 41.

Kocha Msaidizi wa Namungo, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema kuwa “Lusajo ni mshambuliaji bora wa Tanzania na timu ya taifa hivyo ataendelea kuwa bora.
“Kilichomkwamisha msimu huu ni majeraha ya misuli aliyokuwa nayo, kama mnakumbuka aliitwa kwenye timu ya taifa lakini alishindwa kujiunga na timu hivyo huenda angekuwa bora sana.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.