Ni kweli Neymar Jr anatupenda? Binafsi naona ni mapenzi ya mashaka, kaamua kutupa pesa wakati amelewa, pesa hii tuna hofu ya kuitumia kwakuwa ni mlevi huenda kesho akaamka na kutudai pesa yake, nina wasiwasi moyoni
Neymar katukopesha mabao 61 kwenye mechi 101 pale Brazil, anamfukuzia Pele mwenye mabao 77, pale Barcelona kapiga mabao 105 na Assists 77 kwa mechi 186 tu ila PSG kaweka mabao 69 kwenye mechi 80 na Assists 39, ni takwimu bora sana ila najua kalewa nahofia sana kujidai kijiweni
Tukitaka kujua kuna umbali gani kati ya jana na kesho hapo ndipo moyo wangu unateseka zaidi, Neymar leo atamka mzima ila jioni ataumia, tutamkosa Kijiweni kwetu kwa siku nyingi, Neymar leo atakua sawa ila kesho atampiga mtoto wa Mjumbe wa mtaa kisha atapelekwa rumande, hatabiriki huyu, jana na kesho ipo kichwani mwake, Nidhamu tatizo
Lakini vipi kuhusu kumbukumbu atakazotuachia fundi huyu kutoka mitaa ya Mogi da Cruzes pale Sao Paulo?? Binafsi nawaambia wanangu Kijiweni bila wasiwasi naona Neymar anaturudisha kule tusipotaka kukumbuka
Anatukumbusha Andy Van der Meyde, yule fundi winger wa Ajax watu walishakesha Bar kusifia kipaji chake, pale Amsterdam ukitaja jina lake hivi sasa wanaishia kulia tu, Fundi aliishia kula unga na bangi, Neymar atatuachaje wanangu hapa Kijiweni??
Neymar huenda akatuacha na stori kama ya Ricardo Quaresma, fundi wa Kireno aliyekubali kuondoka Barcelona kumpisha Deco, aliamua kutukosesha ladha yake, na vipi kuhusu Adrian Mutu fundi wa Romania??
Siku Neymar akitangaza kutundika daruga atatuachaje, inauma sana kumpenda mtu ambaye hatupendi,
David pere
Neymar anaonekana ni mtu wa starehe Sana Sasa atakapotundika daluga ataendelea kutumia pesa mpaka atafilisika,
winfrida
anapesa nyingi ndomana anazigawa,ila ipo siku atazikumbuka izo pesa anazozitupa
Samiah
Pesa nyingi ndomana anazimwaga
Hope mwaikuka
Atajua yy na sifa zake
Rehema
Naymar anaonekana ni mtu wa starehe
Salma
Watu wrote awawez kufanana
Antony Luseno
Itakuwa ni mapema mno kwa yeye kufanya maamuzi hayo lakini si ajabu kwa wachezaji wanaotokea america kusini uwa wanaendekeza sana starehe
Agness
Kutoa ni moyo mwacheni agawe.
Neema hassan
Neymar anapenda sifa saana..
aisha
Duuh Neymar mtu mbaya 😀😀😀😀😀😀😀
Rehema Dickson
Ni mapema sana kwa yy kufanya maamuzi hayo
Theckla
Neymar ni mchezaji mzuri Sana shida yake anapenda Sana ubishoo
Tahiya
Ni maoni ya mwandishi ila kama itatokea ivyo basi atabaki kwenye vichwa vyetu kama mchezaji mahili na aliyejaribu kuvunja rekodi ya pele japokuwa anaweza kuvunja sababu muda bdo anao
felister
tatizo la neymar ubishoo umemjaa
Mwanaidi
Ni pesa zake na matumizi ni yake haina shida hata kama akizigawa au akiwa na matumizi mabaya
Ester mmakasa
Hawezi kuwaacha kama mnavodhani Kwani neymar hapendi mashabiki wake ?anawapenda sana hawezi kuwaangusha.
Mariam mtandama
Duuuh
Frank Patrick
Kaiacha tuzo yake ya mchezaji bora Barca kafauta pesa huyu fundi wa mpira
Warda
Ndo hivyo tena tupambane na hali zetu#Meridianbettz
Lombo
neymar yuko poa ila ubishoo ndo unamkost yaonekana kama vile mtu mwenye kupenda sana mshahara kuliko kaz
Emmy cleopa
neymar yuko vizur ila Tatizo ubishoo starehe zimemzidi sana
Elika
Huyo Neymar starehe zimemtawala cha msingi achague moja….starehe ama kazi
Gabriel
Neymar n mchezaji mzur ila starehe zimemzid
Lydia Emmanuel Magoti
Neymar yupo vizuri anajua ila anapokwenda Sasa sipo atakifanya kipaji chake kishuke naizo pesa zake Zita muweka pabaya asipo angalia atajiweka sehemu mbaya
Amani
Neymar atatuachaje wanangu hapa Kijiweni#meridianbettz
Caroline
Sidhani kama hayo maneno yana ukweli..
Furahav
Tatizo anapenda starehe sana kuliko mpira.
Hamidu
Neymar ni mchezaji mzuri Sana Ila tatizo mtu wa Bata Sana#meridianbettz
Mwajuma
Neymar atakuwa na matumizi mbaya ya fedha zake kwa maana amezipata kwa njia ya ulaghai
Sadick
Tatizo la Wabrazil wengi ni kupenda starehe wakishaanza kupata fedha#meridianbettz
mwakalosi
huyu Neymar mpira umeshakwisha hakuna chochote zaid ya kuuza,sura na kucheza,na majukwaa
Povel
Shda Neymar jr kaacha kucheza mpr ulaya kaenda kutafut pesa Ila bdo ni fundi wa mpr
Shafii
Ni mchezaji mzuri ila majeraha ya Mara kwa mara ndo maisha yake kwenye career yake
Ernest
Ukweli ni kwamba Neymar ni Talented player na amefanya mambo makubwa lakini kuna vitu vitamfanya asiweke alama kubwa kama wa Brazil wengine.
dorophina
Talent player
Magdalena
Neymar ni mzuri anajua kuucheza mpira shida ubishoo na sifa ndo zinamponzaga
Genia Sikaluzwe
Ni mchezaji mzr lkn bishoo,anaweza kucheza mpira mwenye kiwango km Cha Messi na Ronardo
Isaya massawe
Neymar ubishoo utamfanya apotee mapema kwenye soka
Ester jackson
Binafsi nawaambia wanangu Kijiweni bila wasiwasi naona Neymar anaturudisha kule tusipotaka kukumbuka mana wakali wetu wote wamestahafu na umri umewapa mkono neymar namkubali sana
Kenani
Ameumis uwanja akikanyaga nyasi naona atakiwasha baraa