Jurgen Klopp huyu ni mkombozi wa mbalii anatoka ng’ambo kuja kusaidia watu , kama vile alivotumwa Musa kukomboa wana wa Israel kutoka utawala wa kimabavu pale Misri chini ya mtawala Farao . Kama vile Sam Allardyce au Big Sam yeye ni mkombozi maarufu pale England ajira zake ni maarufu saana mwanzoni mwa mzunguko wa pili , wale walio dhohofu sanaa kushuka daraja hili ndo kimbilio lao . Roberto Di Matteo nae alikua mkombozi wa mbali , alikuja akaichukua timu kutoka shimoni akaipa UEFA na Fa , hawa ni wakombozi huwa wanakuja wanakupa kitu wanasepa , kumpa Big Sam msimu mzima sio nzuri kiafya.
Jurgen Klopp huyu ndie mkombozi wa Ng’ambo mwingine , huyu ndie mkombozi anayependwa zaidii duniani yaani ni mkombozi asiye na makuu pia ambaye hana gharama . Mkombozi asiye na kelele na akiondoka lazima mtamlilia lakini atakwenda na hatarudi , mikono ya kwaheri itamtoa machozi na vilio vya mashabiki vitamuumiza lakini atakwenda na wala hatarudi . Unaweza usielewe lakini angalia jinsi mashabiki na wachezaji wa FSV Mainz 05 walivyolia kwa uchungu sanaa , angalia ambavyo Dortmund walivyomlilia siku ya kuondoka . Rais wa Borrusia Dortmund Reinhard Rauball aliwahi nukuliwa akisema moja ya vitu wanavyojutia ni kumruhusu Jurgen Klopp aende….
Baada ya kuitumikia kwa muda mrefu timu ya FSV Mainz 05 kama mchezaji , lakini mwa 2004 aliipandisha timu hiyo daraja kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu yao . Licha ya udogo wa klabu hiyo , udogo wa uwanja pia hawana hela lakini Klopp alifanya Mainz iwe tishio Bundersliga pia aliiwezesha kufuzu michuano ya Europa kabla ya kutolewa hatua za mwanzoni kabisa na Sevilla . Timu ilivoshuka daraja aliamua kubaki nayo , lakini alivoshindwa kuipandisha akaamua kuachana nayo , wakazi na wazawa na mashabiki wa klabu na jiji la Mainz walilia kilio kisicho na mwisho . Mkombozi aliamua kuondoka alifunga vioo na kuvaa miwani….
Mkombozi kutoka ng’ambo aliamua kutafuta mnyonge mwingine amsaidie akaibukia Dortmund , Thomas Doll alioneshwa mlango wa kutokea baada ya kumaliza nafasi ya 13 safari ya mafanikio ikaanza rasmi . Klopp aliamua kuitengeneza Dortmund kuwa tishio barani ulaya achana na ile ile back to back pale Bundersliga mbele ya vigogo Buyern Munich , mkombozi aliamini saana katika vijana na waliampa matunda . Mario Gotze , Nuri Sahin , Marco Reus ,Matts Hummels , Neven Subotic , Roberto Lewandowski na vijana wengine wengii . Baada miaka nane mkombozi alikwenda huku akiacha alama kubwa sanaa pale Borrusia Dortmund walimlilia lakini ndo alikwenda ivo hakuwaza kurudi.
Mwaka 2015 aliingia makubaliano kwenda kuifundisha Liverpool , mkombozi wa ng’ambo alilidhika na project ya mmiliki wa Liverpool na John Henry aliamua kuingia mkataba wa miaka mitatu . Aliitengeneza Liverpool kwenda kua moja na timu hatari duniani msimu wake wa kwanza aliingia fainali mbili japo hakushinda , miaka inavyokwenda mkombozi alionesha mwanga taratibu alianza kujijengea utawala pale , msimu uliofuata aliingia big four tena unaofuata akaingia fainali ya UEFA na Real Madrid kabla ya uzembe na uchawi wa golikipa Lorris Karius walirudi mikono mitupu . Na sasa anaenda kufanya kitu ambacho kilishindwa kufanyika ndani miaka takribani miaka 30 , Klopp hajawahi angushwa na wamiliki hasa linapokuja swala la bajeti kwani huwa hakurupuki , inaonekana mke wa mmiliki wa Liverpool Linda Pizzuti Henry wakati wa ngololo huwa anabana kwa juu mpaka mzee hawi mchache na mvivu kwenye bajeti.
Mkombozi anakwenda kutengeneza kilio kingine , ipo siku atamwaga watu machozi watamlilia lakini atakwenda na hatarudi . Kila palipo na harufu ya Liverpool Klopp anasemwa na anapendwa kuanzia uwanjani mpaka maisha ya kawaida , kuanzia Melwood hadi Anfield jamaa anapendwa sanaa . EPL ya kihistoria anayoenda kuwapa hawatamsahau kamwe kama walivyoshindwa kuwasahau Bill Shankly na Bob Paisley . Siku anayoondoka tutashuhudia mengi saana.
David pere
Alama kubwa ameiweka na ataendelea kuweka Kama ataendelea kuwepo pale EPL
Sadick
Story ya kuvutia sana, Jürgen Clopp ni Kocha na mhamasishaji mzuri. Nataka kuona kama msimu huu ataipa Liverpool Ubingwa baada ya kuukosa kwa miaka 30#meridianbettz
winfrida
jurgen endelea kuwa na moyo huo huo
Samiah
Jurgen clopp nikocha muhamasishaji
Hope mwaikuka
Big up to jurgen
Salma
Nategemea maajabu kwenye msimu huu
Rehema
Jurgen ameiweka na Kama ataendelea kuwepo pole EPL
Agness
Tunategemea afanye maajabu Kama ataendelea kuepo
Antony Luseno
Klopp the master ni kocha ambaye klabu zote duniani zitajivunia kufanya kazi pamoja na yeye
aisha
Juegen klopp ni kocha anaejua
Devotha
Clopp ni kocha mzuri sana ndo maana hupendwa na wengi
Neema hassan
Klopp kocha mahiri saana..
Rehema Dickson
Nataka nione kama ataipa ubingwa Liverpool baada ya kuukosa zaidi ya miaka 30 iliyopita
Adelta
Jurgen aendelee kuwa na moyo huohuo
Tahiya
Mwandishi yuko sahihi sana kumuita mkomboz, mana ameenda kuikomboa liverpool baada ya miaka 30
Theckla
Namkubali Sana Mana ni kocha anejua kupanga mashambulizi kwa wachezaji wake
felister
kocha mwaijibikaji
Ester mmakasa
Duuh! Nimependa sana Jurgen Klopp jinsi anaviishi kiuharisia kuanzia maisha ya kawaida mpka uwanjani ,anafaa kuigwa na kila mtu mwenye malengo.
Mwanaidi
Inapendeza sana kama ukiacha alama nzuri sehemu na watu wakaendelea kukukumbuka big up kwake
Elika
Habari njema sana hii
Mariam mtandama
Habari mjema
Frank Patrick
binafsi machozi yatanidondoka ….YNWA tunashukuru ameongeza mitatu mingine..Klopp is Kop
Warda
Kweli anapaswa kuliliwa #Meridianbettz
Lombo
Jurgen klopp yuko vema sana namkubali
Emmy cleopa
Habari njema sana hii
Gabriel
Still bado klopp n kocha mzur sana tnx # meridianbettz
Lydia Emmanuel Magoti
Jurgen Klopp yupo vizuri tumpe pongez zake kwakweri
Amani
Klopp hajawahi angushwa na wamiliki hasa linapokuja swala la bajeti kwani huwa hakurupuki
Furahav
Huyu jamaa ni kocha mzuri sana.
Caroline
Jurden Klopp ni mtu Mzuri sana
mwakalosi
klopp ni bonge la kocha ambaye anafit kwenye mifumo yote kwa sasa
Hamidu
Bonge la Coach.. klopp fundi wa mbinu katika uwanja#meridianbettz
Mwajuma
amefanya mambo makubwa sana pale liverpool na EPL kwa ujumla ndio maana kila sehemu kaacha alama
Shafii
Klop namkumbali ni kocha mzuri sana
Ernest
Klop ni kocha bora sana katika karne hii
Povel
Klopp ni moja Kati ya makocha Bora hv hv Sasa ulaya na dunia na mipaka yake
dorophina
Ni kocha mzuri sana na anambinu zote katika mpira
Magdalena
Klopp alikuwa mahili mzuri ndo maana kila alipokuwa anakanyaga aliacha alama nzuri
Genia Sikaluzwe
Klopp ni kocha mzuri,anajua kuishi na wachezaji ndio maana Kila anapopita anaacha alama
Kenani
Ni kocha wa tofaut mwenye upeo tofaut wa kuona mbali
Issa
Klopp ni kocha makini sana anajua kuibua vipaji anajua kumkomaza mchezaji