Tetesi zinasema, Mshambuliaji wa Ubelgiji Romelu Lukaku hana nia ya kujiunga na AC Milan ama Newcastle msimu huu wa joto, licha ya mchezaji huyu mwenye umri wa miaka 28-kuendelea kukosa nafasi ya kucheza katika klabu ya Chelsea.
Tetesi zinasema, Barcelona itapokea ofa za pesa nyingi kwa ajili ya kiungo wa kati wa Uholanzi Frenkie de Jong. United wamehusishwa na mchezaji huyo wa miaka 24.
Newcastle wanamtaka mshambuliaji wa kimataifa wa Benfica na Uruguay Darwin Nunez,22, ambaye anahusishwa na Manchester United na Liverpool.
Kocha wa Tottenham, Antonio Conte anapania kuimarisha kikosi chake msimu huu wa joto kwa kuwasajili kiungo wa kati wa Southampton na Uingereza James Ward-Prowse, 27, na beji wa kushoto wa Brighton na Uhispania Marc Cucurella, 23.
Tetesi zinasema, Chelsea wanataka kumsajili mlinzi wa Croatia Josko Gvardiol, 20, kutoka RB Leipzig huku Antonio Rudiger, 29, na Dane Andreas Christensen,26, wakitarajiwa kujiunga na Real Madrid na Barcelona.
Inter Milan wako tayari kumuuza Stefan de Vrij kwa £15m msimu huu wa joto, huku Tottenham, Aston Villa na Newcastle zikiwa miongoni mwa vilabu vinavyomhitaji mlinzi huyo.
Arsenal watafanya jaribio la mwisho la kumuongeza mshambuliaji wa Uingereza Eddie Nketiah, 22 kwa mkataba mpya, mkataba wake wa sasa unamalizika mwishoni mwa msimu.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.