Trent Alexander Arnold- Kizazi Kipya cha Mabeki Wanaoshambulia

Trent anakuja kutupa somo jipya namna mpya na darasa jipya , anakuja kutupa vitu ambavyo hatukuviona kwa muda kidogo beki wa kulia mwenye takwimu nyingi za hatari za kushambulia kuliko kukaba . Wapo wanaosema kijana anasweet zaidi akicheza kama kiungo lakini Klopp bado hajaamua iwe ivyo , kuna waliomshuhudia Dani Alves pia wapo waliomfaidi Phillip Lam , unaweza changanya utamu wao ukampata Trent.

Soka la kiingereza lilikua na ustaarabu wake kabla ya kuja Arsene Wenger na pasi zake nyingi , mara nyingi build up ya magoli ilianzia pembezoni mwa uwanja , watakuja kupitia pembeni na kupiga mashuti au watapiga krosi nyingi . Arsene Wenger alikuja na utamaduni wake kwanza lazima timu imiliki mpira ndipo wamfuate mpizani kwa hatua lakini aliposhindwa kujiongeza ukawa mwisho wake , kwa sasa hata Guardiola ameamua kuwaiga wazawa magoli yake mengi yanatokea pembeni kuliko katikati .

Trent Alexander Arnold

Pengine Dani Alves anaweza kua moja ya mabeki wa pembeni wa kulia bora kabisa kuwahi kutokea , jamaa aliweza kila aina mchezo kuanzia pasi fupi fupi pia anazijua one-two vizuri anapiga krosi za uhakika pia ni fundi wa mipira iliyokufa , kuna Phillip Lam naye anaingia humo hata Cafu anajaa humo kiuhakika . Wote hawa walitupa aina tofauti ya mlinzi wa kulia hadi kila mtu akasema yake , lakini Jurgen Klopp amekuja na aina yake ya kipekee , kifupi wote hao Alves na Lam wanajua kuchezesha timu ila Trent ni darasa jipya.

Andrew Pirlo aliitwa Deep Lying Playmaker huyu alikua kiungo mshambuliaji lakini alianzia harakati zake nyuma kabisa , tukumbuke tu Pirlo alikua kiungo ina maana hizo harakati alizifanyia akiwa kama kiungo . Baada ya kumtathmini sana Trent leo nimeliona jina jipya sehemu na anaitwa DEEP LYING WIDE PLAYMAKER , ndio inabidi aitwe ivyo hakuna namna kijana anakosa sifa za kiulinzi ila anasifa za kwenda mbele zaidii , Trent mpe pasi hata akiwa eneo lake la hatari atafanya jambo zuri tu ila mwambie akabe ndani ya eneo la hatari utampa lawama za bure.

Trent Alexander Arnold

Ujio wa kiungo fundi mkabaji wa Kibrazil Fabinho Travarez ndio ulimfungulia Trent dunia kua anachotaka , iko ivi ili unyonye uwezo woote wa Trent lazima pawe na mtu anakaeziba nafasi yake wakati yeye ameenda kufanya anachotaka . Alikuwepo Emre Can huyu jamaa alikua kiungo mzuri sanaa na alikua mkabaji lakini alipenda sana kushambulia alafu alikua homa za vipindi , Jordan Handerso hakuonekana kuwasoma wapinzani kiulinzi hata kushambulia hakuwasoma lakini ni nahodha . Pengine Trent na Robbo ndio vijana hatari sana kwa sasa lakini hatuangalii kina nani wanawapa hua uhatari , uwepo wa fabinho pale Liverpool ndio unaleta usawa sana na timu kupata balance.

Trent anakupa vitu vingi sana mpaka raha kwanza ni fundi sanaa wa kupiga pasi ndefu kiustadi yeye kuhamisha uwanja ni kama kunywa maji , ukimmark sana basi anaanza kupia one-two sababu yupo huru sana na mpira , trent ni mjuzi wa kukimbia kuziwahi pasi iwe kwa kuingia ndani ( underlap ) au pembezoni mwa touchline ( overlap ) , kuna muda anaungana na viungo kama pembeni kumebana sana , anapiga mipira iliyokufa kwa umahiri wa hali ya juu , anatengeneza nafasi za kufunga kwa umahiri mkubwa pia ana mguu mzuri wa kufunga.

 

57 Komentara

    klopp hapa alilamba dume na kumaliza mchezo

    Jibu

    Ni beki mzuri Sana

    Jibu

    Trent yuko vzur sana na sifa ya kupiga pasi ndefu ndo usiseme fundi sana huyu jamaa

    Jibu

    Uko vzr ni kocha mzr

    Jibu

    Trent Arnold yupo vzr sana kwny kushambulia Ila kwny kukaba ndo tatizo thnks meridian bet kwa gud news

    Jibu

    Mchezaji mzuri sana

    Jibu

    Hatari sana Anord.

    Jibu

    Beki yuko vizur sana

    Jibu

    Dogo anajua Sana kutimiza majukumu yake akiwa uwanjani

    Jibu

    Yupo vizuri

    Jibu

    Mzur

    Jibu

    Yup vizuri sana

    Jibu

    Asanten kwa taarifa meridianbet

    Jibu

    anatengeneza nafasi za kufunga kwa umahiri mkubwa pia ana mguu mzuri wa kufunga.#meridianbettz

    Jibu

    Trent yupo vizuri

    Jibu

    klop alipata beki mshambuliaji, ambaye anakila kitu awapo uwanjani, kila mmoja anamuonaga Anord awapo kiwanjani hatanii kazikazi tu. #meridianbet

    Jibu

    Yuko vizur

    Jibu

    Yuko vizuri

    Jibu

    Ni beki mzuri sana

    Jibu

    kisik

    Jibu

    Nibeki anaejielewa nin anafanya

    Jibu

    Dogo yupo vizuri Sana anajua jinsi gani ya kujitengenezea nafasi ya kufunga magoli

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Namkubar Sana uyo jamaa

    Jibu

    Beki mkali

    Jibu

    Yupo vizuri sana

    Jibu

    Mfumo wao wa uchezaji uwa unasaidia kuipa timu matokeo

    Jibu

    Ni beki poa sana

    Jibu

    Bonge moja la beki

    Jibu

    ni beki nzuli#meridianbettz

    Jibu

    Yupo vizuri sanaaa

    Jibu

    A.A.. mkali wa assist pale EPl .! Dogo mnamkubali Sana# meridianbettz

    Jibu

    Ni beki hatari

    Jibu

    Thnks meridian bet tz kwa gud news

    Jibu

    Nibek mzuri sana

    Jibu

    Klopp amchezeshe midle dogo kama Stevie G

    Jibu

    Anord Ni miongoni mwa wanaoleta mafanikio ya liverpool

    Jibu

    anajua nini anachofanya

    Jibu

    Anajitahidi sana huyu beki na anafanya vizuri

    Jibu

    Beki mzuri sana

    Jibu

    Ni makala nzuri sana kwa watanzania wote wenye malengo na wenye vipaji kama hawa walioandikwa makalani ,tujifunze na tufanyie kazi .

    Jibu

    liver wanajivunia kuwa na beki bora

    Jibu

    Ni beki makini uyu

    Jibu

    Mchezaji mzuri lakini hafai kuwa beki #Meridianbettz

    Jibu

    Anajua nini anachokifanya

    Jibu

    Trent ataweka record kubwa sana kwenye ulimwengu wa soka endapo tu ataendelea kukaza Buti.

    Jibu

    Ni beki bora timu ikiwa inashambulia

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Club ya Simba ilikuwa inamtaka huyu #Meridianbettz

    Jibu

    Beki mkali sana

    Jibu

    Yuko vizuri

    Jibu

    Yuko poa sana

    Jibu

    Bekii makinii sana

    Jibu

    Beki Yuko poa sana

    Jibu

    Trent fundii

    Jibu

    Arnold ni mahiri na beki mpambanaji

    Jibu

    Trent yupo vzr Sana ni beki bora hajawahi kuiangusha timu yake Safi Sana hongera klopp kwa kupata beki mzuri

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.