al-Hilal Wapiga Pini MechI Yao Dhidi ya Yanga Kuoneshwa.

Klabu ya Al-Hilal ya Sudani imegoma mechi yao ya mzunguko wa pili wa ligi ya Mabingwa Afrika katika hatua ya awali ya ligi baada ya mchezo wa kwanza kupigwa katika uwanja wa Benjamin Mkapa.

AL-HILALBaada ya mchezo wa kwanza kumalizika jijini Dar-es-salaam kwa sare ya goli moja kwa moja na mchezo wa pili utapigwa katika jiji la Khartoum nchini Sudani katika dimba la Omdurman kati ya Al-Hilal dhidi ya Yanga.

Katika mchezo huo ambao inaelezwa klabu ya hiyo imegomea kiasi cha milioni 200 kutoka kwa kampuni ya kurusha matangazo ya Azam Media na kutohitaji mchezo huo kurushwa mubashara kutoka nchini Sudani.

Hali imewashangaza watu wengi lakini ikumbukwe katika hatua za awali na hatua za kwanza klabu ndio ina haki ya matangazo ya michezo yao hivo shirikisho la mpira barani Afrika halina nafasi na nafasi yao inakuja kuanzia hatua ya makundi.AL-HILALMpaka sasa haijafahimika sababu za msingi za klabu ya Al-Hilal kwanini inagomea mchezo huo kurushwa mbashara.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.