Kagera Wahamishwa Mwanza

BODI ya ligi kuu (TPBL) limeihamisha timu ya Kagera Sugar Jijini Mwanza kwenye Uwanja wa CCM Kirumba baada ya uwanja wao kuwa na mapungufu.

Kagera imeutumia uwanja wao wa Kaitaba leo kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Singida Big Stars.

Barua kutoka TPBL iliyotolewa leo imeeleza kuwa timu hiyo itautumia uwanja wa CCM Kirumba uliopo Mwanza kutokana na marekebisho mbalimbali kutokamilika.

Marekebisho hayo ni kutokuwepo kwa uzio wa kutenganisha mashabiki na eneo la kucheza hivyo kuhatarisha usalama wa wachezaji.

Kamati ya leseni za klabu itaruhusu uwanja huo kutumika baada ya kuukagua na kujiridhisha kuwa mapungufu hayo yamerekebishwa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.