Baada ya kuwepo sintofahamu kuhusu hatima ya Kyrie Irving kunako Ligi ya NBA msimu huu. Hatimaye, Irving amerejea uwanjani 2022.
Kutokana na kuweka mgomo wa kutochanja chanjo ya COVID-19, uongozi wa klabu ya Brooklyn Nets, uliweka bayana (kupitia kocha mkuu wa timu hiyo) kuwa, Irving hatoruhusiwa kuitumikia timu hiyo kama hajachanja.
Pamoja na tamko la uongozi wa timu, mamlaka za jiji la New York, zilitoa tamko kwa wanamichezo wote, kama hujachanja, hutoruhusiwa kushiriki michezo ndani ya jiji hilo.

Muda ulikwenda, Irving akaendelea kua nje ya uwanja toka mwezi Juni. Mwezi Disemba, Nets waliamua kumruhusu mchezaji huyo kurejea kwenye timu yao na kuwa miongoni mwa wachezaji watakaotumika msimu huu.
Mchezo wa kwanza kwa Kyrie Irving umeangukia dhidi ya Indiana Pacers. Kyrie hajarudi kinyonge, mchezo unatamatika kwa Nets wakiibuka kidedea kwa pointi 129-121 huku Irving akipachika jumla ya pointi 22.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


