NBA: Lakers na Warriors Waangukia Pua.

Msimu mpya wa NBA umefungulia usiku wa kuamkia leo. LA Lakers walikuwa uwanjani kupambana na LA Clippers wakati ambapo Brooklyn Nets walichuana na Golden State Warriors.

Lakers walijukuta wakipoteza mchezo dhidi ya Clippers baada ya kumaliza mchezo kwa pointi 109-116. Alikuwa ni Paul George aliyeng’ara kwenye mchezo huo baada ya kuipatia Clippers pointi 33 kabla ya Kawhi Leonard kuongeza zingine 22 katika kipindi cha pili.

Hii ni mara ya pili mfululizo kwa LA Clippers kushinda mechi ya kwanza kwenye misimu ya NBA.

Paul George (katikati) akiwasumbua walinzi wa LA Lakers.

Upande wa pili, Kevin Durant aliiongoza Brooklyn Nets kwenye mchezo dhidi ya timu yake ya zamani – Golden State Warriors.

KD alijiunga na Nets kwa mkataba wa miaka 4 akitokea Warriors 2019. Licha ya kutoitumikia Nets kwa sehemu kubwa ya msimu uliopita baada ya kupata majeruhi, KD aliisaidia Nets kuibuka na ushindi wa pointi 125-99.

Durant alipachika pointi 22 wakati ambapo mpinzani wake Stephen Curry aliisaidia Warrior kupata pointi 20 na alitoa pasi 10 za magoli.

Kevin Durant akiwaadhibu Golden State Warriors na kupeleka ushindi Brooklyn Nets.

Akizungumzia kurejea kwa KD kwenye msimu huu wa NBA, kocha wa Brooklyn Nets – Steve Nash alisema, “Kuna tofauti kubwa sana ya kuwa nje ya NBA kwa miezi 18 na ukarejea tena baada ya yote aliyoyapitia.

“Anaonekana kama Kevin, anacheza kama Kevin lakini sitaki kuweka matarajio yangu kwake mpaka pale atakapokuwa vizuri zaidi na atakapozoea kucheza mechi 3 ndani ya siku 4.

“Kwake ndio hatua inayofuata. Tunapaswa kumtizama siku baada ya siku.”

LeBron James akiwa na pete ya ubingwa wa NBA.

Licha ya kupoteza mchezo wa kwanza, kama ilivyodesturi ya mashindano hayo – bingwa watetezi [LA Lakers] walikabidhiwa pete zao za ubingwa kabla ya mchezo.

Pete za Lakers zimeweka picha ya Mamba kama sehemu ya kumuenzi gwiji wa timu hiyo – Kobe Bryant ambaye alifariki kwa ajali ya chopa mapema mwezi Januari.

Pete hiyo pia imewekwa namba 8 na 24 zikiwa ni namba za jezi alizowahi kuzitumia Bryant wakati alipokuwa na timu hiyo pamoja na kuwekwa nakshi ya jezi ambazo zimestaafishwa na timu hiyo.


VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!

Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???

SOMA ZAIDI

14 Komentara

    Kevin yuko vizuri ila aongeze juhudi

    Jibu

    Lakers mmeniangusha chama langu

    Jibu

    Lakers nilitegemea ushindi

    Jibu

    Lakers mmeharibu Kila kitu

    Jibu

    Lakers wanakwama wapi

    Jibu

    Nic

    Jibu

    Lakers wameanza kupotea

    Jibu

    Ilkua siku mbaya kwa lakers

    Jibu

    Lakers mmezingua sana

    Jibu

    Lakers wanakwama wapi

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Haikuwa kazi laisi kwao Lakers

    Jibu

    Huwezi kuwa juu kila siku

    Jibu

    Sio mbaya mwanzo mgumu

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.