Mvutano wa taji la AFCON 2025 umeendelea kupamba moto huku timu ya taifa ya Senegal ikionyesha msimamo wake wazi kabla ya mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Peru.
Kuelekea mchezo huo utakaopigwa kwenye uwanja wa Stade de France, Senegal imeweka bango lenye nyota mbili kwenye eneo la benchi la ufundi na njia ya kutokea wachezaji (tunnel), hatua inayotafsiriwa kama ishara ya kujitangaza kuwa mabingwa wa mara mbili.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Hatua hiyo imekuja katikati ya mvutano unaoendelea na CAF kuhusu uhalali wa mataji hayo, jambo ambalo limeibua mjadala mkubwa miongoni mwa wadau wa soka barani Afrika.
Chanzo kutoka ndani ya timu Senegal kilinukuliwa kikisema, “Hii ni njia yetu ya kuonyesha tunachokiamini. Tunaamini sisi ni mabingwa na tutasimama na hilo.” Kauli hiyo inaonyesha dhamira ya Senegal kusimamia msimamo wao licha ya utata uliopo.
Wachezaji, benchi la ufundi pamoja na mashabiki wa Senegal wanatarajia kufanya sherehe za ubingwa ndani ya uwanja huo, wakilenga kuonyesha umoja na kuondoa sintofahamu iliyotokana na mzozo huo.
Mchezo kati ya Senegal na Peru unatarajiwa kuchezwa leo Jumamosi, Machi 28, 2026 majira ya saa 11:00 jioni kwa saa za Tanzania, huku ukiwa si tu mtihani wa kirafiki bali pia jukwaa la Senegal kuonyesha nguvu na msimamo wao mbele ya dunia.

