Kounde Amekiri Kwamba Anaweza Kusepa Sevilla

Mlinzi wa Sevilla Jules Kounde amekiri kwamba anaweza kuondoka katika klabu ya Sevilla wakati wa mapumzimko hali yakuwa amekuwa akihusishwa na klabu ya Manchester United.

Kounde Amekiri Kwamba Anaweza Kusepa Sevilla

Kounde ameibuka kuwa mmoja wa mabeki wa kati wanaotafutwa sana katika soko la uhamisho baada ya Dayot Upamecano kujiunga na Bayern Munich na Ibrahima Konate kukubali kubadilishana RB Leipzig na Liverpool.

Kwa muda mrefu United imekuwa ikihusishwa na uhamisho wa Kounde, ambaye aliisaidia Sevilla kumaliza katika nafasi ya nne katika LaLiga msimu huu, kwani vigogo wa Ligi Kuu ya Ole Gunnar Solskjaer wameripotiwa kumtazama beki mpya atakaye saidiana na Harry Maguire.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 22 – pia anayeripotiwa kulengwa na vilabu kama Real Madrid, Chelsea na Arsenal – alisema anataka kushinda mataji.

Kounde Amekiri Kwamba Anaweza Kusepa Sevilla

“Kuhusu mustakabali wangu, huenda nikabadilika msimu huu wa joto,” Kounde aliwaambia waandishi wa habari wakati Ufaransa ikijiandaa kwa mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Wales Jumatano, kabla ya Euro 2020 inayokuja.

“Bado hakuna ukweli wowote, sijafanya uamuzi wa mwisho.

“Ni wazi, lengo langu ni kucheza siku moja katika moja ya vilabu vikubwa ili kuendelea kuimarika na kushinda mataji.


BONASI YA 50% KILA SIKU KATIKA KASINO ZA EVOPLAY HAPA MERIDIANBET.

Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.

tuchel, Tuchel :Tuna Bahati Tottenham Wametusaidia Kazi., Meridianbet

SOMA ZAIDI

5 Komentara

    Kwenye usajiri mwenye kisu kikali ndio anakula nyama

    Jibu

    Kazi ya ziada ipo

    Jibu

    Sola letu bhana!!!!

    Jibu

    Kazi ipo

    Jibu

    Safi asep

    Jibu

Acha ujumbe