Simba Yanguruma Lilongwe.

Simba imefanikiwa kupata ushindi wa magoli mawili kwa bila katika mchezo wa awali waligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Nyassa Big Bullets ya nchini Malawi katika mchezo uliopigwa katika dimba linalofahamika kama Bingu National stadium nchini humo.

Vijana hao wa Juma Mgunda wanapata matokeo dhdi ya mabingwa hao kutoka nchini malawi mara baada ya kulazimishwa suluhu katika mchezo wao wa ligi kuu Tanzania bara baada ya kulazimishwa sare ya goli mbili kwa mbili na klabu ya KMC jijini Dar-es-salaam.

simbaSimba ambao wamekua wazoefu katika michuano hii sasa walipata goli lao la uongozi kupitia kwa mshambulia wao raia wa Zambia Moses Phiri akiwa anafunga goli lake la nne katika michezo minne aliyocheza hadi sasa huku goli la pili likifungwa na nahodha wa timu hiyo mkongwe John Raphael Bocco.

Klabu hiyo inapata matokeo mazuri ikiwa ugenini kitu ambacho kinawweza kuwakikishia kusonga mbele kwenye hatua nyingine ya michuano kwani imekua nadra sana kwa klabu hiyo kupoteza mchezo wakiwa katika dimba lao la nyumbani.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.