Aston Villa walimfungasha vilago kocha wao Dean Smith na kufanya awe ni kocha wa tano msimu huu kutimuliwa na vilabu vya EPL baada ya Xisco Munoz (Watford), Nuno Espirito Santo (Tottenham) , Steve Bruce (Newcastle) na Daniel Fark (Norwich) kufutwa kazi na vilabu hivyo kufuatia matokeo duni ya timu.

Sasa wachezaji wazamani wa timu ya taifa ya Uingereza John Terry, Steve Gerrard na Frank Lampard wote wamehusishwa na kuirithi mikoba ya Smith huko Villa Park.
Villa wameamua kutafuta suluhisho na kuleta mabadiliko chanya kwenye kikosi chao baada ya kukaa nafasi ya 16 baada ya michezo 12 ya Premier League na wamefikia uamuzi wa kumfuta kazi Smith baada ya kupoteza katika michezo mitano mfululizo ya ligi.

Terry alichaguliwa kuwa kocha msaidizi wa Dean Smith mwaka 2018 na kusadia Villa kupanda daraja la Ligi kuu na aliachana na timu hiyo wakati uliyopita wa majira ya joto, kwa namna hiyo anaweza kuwa mbadala thabiti wa Smith.
Steve Gerrard kwa sasa ni kocha mkuu wa Rangers ambaye amewapa taji la Scotish Premier League kwa mara ya kwanza ameripotiwa kuwa kwenye mkataba na klabu hiyo mpaka 2024.
Frank Lampard baada ya kutimuliwa na Chelsea mwezi Januari anaweza kurejea kwenye ukufunzi na timu ya EPL licha ya kushindwa kuleta matokeo mazuri darajani lakini Redkanpp anaamini Lampard ana uwezo wa kupata mafaniko katika kazi ya ukocha.
NJIA RAHISI YA MKWANJA NA TITAN DICE
Unawezaje kuikosa hii! njia rahisi ya kutengeneza mkwanja katika kasino maridhawa za meridianbet. Muda wa kufurahia na kutengeneza mkwanja ipo mikononi mwako unasubiri nini?


