Mgunda Awashushia Lawama Washambuliaji Wake

Kocha Mkuu wa kikosi cha Simba, Juma Mgunda amepeleka lawama zake kwa mastraika wa timu hiyo kutokana na kushindwa kuzitumia nafasi walizopata.

Simba walipoteza mchezo wa ligi dhidi ya Azam jana alhamis kwenye Uwanja wa Mkapa, kwa bao 1-0 likifungwa na Prince Dube.

Akizungumzia matokeo hayo Mgunda alisema: “Kwanza namshukuru Mungu mchezo umemalizika salama, tumejitahidi kwa ajili ya kuhakikisha tunashinda mchezo lakini imeshindikana.

“Mchezo ulikuwa mzuri tumetengeneza nafasi nyingi za wazi lakini tumeshindwa kuzitumia, wenzetu wametengeneza nafasi na wameitumia hivyo ndivyo mpira wa miguu ulivyo.

“Tunarejea mazoezini kwa ajili ya kurekebisha hayo makosa yaliyojitokeza kwenye mchezo wa leo ili yasijirudie tena.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.