Polisi Kuipeleka Simba Ushirika

Mchezo wa ligi kuu kati ya Polisi Tanzania dhidi ya Simba unaotarajiwa kuchezwa Novemba 27 mwaka huu utapigwa kwenye Uwanja wa Ushirika, Moshi.

Polisi Tanzania kwa msimu huu wametumia viwanja mbalimbali ikiwemo uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha na Black Rhino Academy, Karatu baada ya uwanja wao kufungiwa.

Akizungumzia kurejea kwenye Uwanja wao wa nyumbani, Ofisa Habari wa Polisi Tanzania, Hassan Juma amesema: “Mchezo unaofuata tutacheza ugenini dhidi ya Ihefu kwenye Uwanja wa ugenini.

“Kikosi kinaendelea na maandalizi kuelekea kwenye mchezo huo, japo hatukuwa na matokeo mazuri kwenye mchezo uliopita lakini bado wachezaji wana morali kwa kuhitaji kuonyesha kile wanachokitamani.

“Tunatarajia kurejea hivi karibuni kwenye Uwanja wetu wa ushirika kutokana na matatizo ambayo tunakutana nayo ya viwanja tunavyotumia kufungiwa.

“Mchezo dhidi ya Simba ambao tutakuwa kwenye Uwanja wa nyumbani tutaanza kuutumia uwanja wa Ushirika pamoja na michezo mingine iliyobaki ya nyumbani.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.