Hiannick Kamba 🇨🇩 apatikana tena Baada ya Kutangazwa Kufariki Katika Ajali ya Gari Mnamo mwaka 2016. Mchezaji wa zamani wa klabu ya Schalke 04, Hiannick Kamba amepatikana akiwa hai nchini Ujerumani ikiwa ni miaka minne baada ya kutangazwa kuwa amefariki katika ajali ya gari.

Mnamo Januari 2016 Kamba aliripotiwa kupata ajali ya gari akiwa nchini kwao Congo na klabu yake ya wakati huo, VfB Huls, ilisema kwamba mchezaji huyo alikuwa amepoteza maisha kwenye ajali hiyo. Kamba ambaye kwa sasa ana miaka 33, ameripotiwa kupatikana akiwa hai katika jiji la Ujerumani la Gelsenkirchen na anaweza kukabiliwa na mashtaka ya kisheria.
Mwendesha mashtaka Anette Milk amefunguka kuwa kesi inachunguzwa dhidi ya mke wa zamani wa Kamba, anayedaiwa kukusanya ‘malipo ya bima ya maisha’ ya mchezaji huyo mara tu baada ya kuripotiwa kifo chake. Anette ambaye ni Mke wa zamani wa mchezaji huyo alidai kuwa anastahili malipo ya bima ya maisha ya mchezaji huyo mara tu alipopata habari ya kifo na alionyesha hati ya kifo kwa kampuni ya Bima.
Bild imeripoti kuwa Kamba atakuwa kama sehemu ya ushahidi katika uchunguzi juu ya udanganyifu ulioweza kutokea. Beki huyo wa zamani wa kimataifa wa Congo, aliwahi pia kucheza na kipa Manuel Neuer wakiwa katika klabu ya Schalke, pia alichezea vilabu vya Ujerumani kama SV Zweckel, SG Borken na Recklinghausen wakati wa maisha yake ya soka.
MCongo huyo kwa sasa anafanya kazi kama Mtaalam wa kemikali kwenye kampuni ya usambazaji wa nishati


SADICK
Duh! Asante meridian kwa habari hii
povel
thnks meridian kwa habari moto moto za kimichezo
Gabriel
Habar ya kushangaza inamaana alizikwa akiwa hai? Au mistake
Neema juma
Aisee kumbe hakufaa kijana wa watu. Taarifa tunazipata huku meridianbet
Tatu
Du kumbe ajafa nashukuru kulifaham hvyo
Elika
Inauma sana kusingiziwa kifo
Mwajuma
Du inashangaza sana
Neema hassan
Daah!inasikitisha Sana…lkn aliwezaje kupata Cheti Cha kifo?
Rehema Dickson
Duu isee hii habari nzito
Khadija
duh Mambo yapo meridian
Furahav
Inasikitisha sana.
Theonestina
Duuuh mwanamke anatamaa sana.najiuliza amewezaje kupata hati ya kifo😲