VIINGILIO vya mchezo wa ligi kuu kati ya Yanga na Simba vimewekwa wazi leo na Shirikisho la Soka nchini (TFF) ambapo kiingilio cha chini ni 5000 tu.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Oktoba 23 mwaka huu kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar ambapo Yanga watakuwa uwanja wa nyumbani.

TFF wameweka wazi viingilio hivyo leo jumatatu ambapo mzunguko itakuwa 5000, machungwa 10000, VIP C 15000, VIP B 20000 na VIP A 30000.
Timu hizo zinashuka dimbani zikiwa na pointi 13 zote huku tofauti ikiwa ni tofauti ya mabao ambapo Simba wakiwa nayo tisa na Yanga akiwa nayo saba.

