BAADA ya kuingia hatua ya makundi ya michuano ya Klabu bingwa Afrika, Kocha Mkuu wa Simba, Juma Mgunda amefurahishwa na viwango vya wachezaji waandamizi ndani ya kikosi hicho.
Simba iliingia hatua ya makundi baada ya kuiondosha Primeiro De Agosto ya nchini Angola kwa jumla ya mabao 4-1.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Mgunda alisema “Kwanza tunamshukuru Mungu kwa kumalizika salama kwa mchezo.
“Pia wachezaji wangu hasa wale waandamizi ambao waliifanya kazi yangu kuwa nyepesi baada ya kufuata maelekezo ambayo niliwaelekeza.
“Wachezaji hao ni pamoja na Clatous Chama, John Bocco na Jonas Mkude ambao walifanya kazi yangu ambayo ilikuwa ngumu kuwa nyepesi.”

