Shangwe Za Ubingwa Simba Zaingia Shubiri

Gari hilo lililofika kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar saa 2:05 asubuhi, liliandaliwa maalum kwa ajili ya wachezaji hao kupanda huku wakisherehekea ubingwa wa huo wa ligi waliouchukua kwa mara ya tatu mfululizo.

Msafara huo wa Simba ulitua kwenye uwanja wa ndege saa 3:00 asubuhi wakitokea Ruangwa, Lindi kabla ya kwenda kupanda ndege Mtwara na kuanza safari ya kurejea Dar wakitoka kucheza michezo yake miwili ya ligi na Ndanda FC, Namungo FC ambayo yote walimaliza kwa suluhu.

Baada ya kuwazuia wachezaji hao kupanda kwenye gari hilo, Sven akatoa maagizo wote wapande kwenye gari aina ya Toyota Coaster ya timu hiyo wanayoitumia U20 na ile ya wanawake.

Baadaye Sven alitoka kwenye mlango mkubwa wa kutokea abiria akiwa amekunja uso na kumfuata msaidizi wa Mtendaji Mkuu (C.E.O) wa timu hiyo, Senzo Mazingisa ambaye ni Rispa Hatibu kisha akamfuata ofisa mmoja wa Simba na kuanza kumfokea kwa sauti kubwa akisikika kuonekana kugomea mapokezi hayo.

“Kitendo hicho kimeonekana kuwakera viongozi hao walioongozana na msafara huo akiwemo Kaimu Rais wa Simba, Kaduguda (Mwina) ambaye yeye mara baada ya kumuona kocha anafoka, akaachana naye akaondoka na usafiri wake,” alisema mtoa taarifa huyo.

Msafara wa timu hiyo ulianza safari ya kutoka uwanja wa ndege hapo saa 3:10 asubuhi kwa Toyota Coaster huku wakiliacha gari la wazi na kuelekea Mbweni Ndege Beach ambako timu hiyo imeweka kambi yake kujiandaa na mchezo dhidi ya Yanga.

46 Komentara

    Simba wako vizuri ….!!!!

    Jibu

    Ahsante kwa taarifa

    Jibu

    Wakifungwa na yanga tu saherehe zote zinakuwa chungu Mana hakuna Raha tena

    Jibu

    Simba ni timu bora kwanza iko vizuri na wachezaji wake wako vizuri

    Jibu

    Nawkubali sana Simba wapo vizuri ⛹️👍

    Jibu

    kocha anaogopa korona

    Jibu

    Simba wako gud

    Jibu

    Homa ya jiji jpili hiyo

    Jibu

    Simba mabingwa Mara 3 mfururizo#meridianbettz

    Jibu

    Simba ni mabingwa mara 3 mfululizo na jumapili lazima tumchape yanga

    Jibu

    Kocha ajakosea yuko sahihi kabisa #meridianbettz

    Jibu

    Simba wako vizuri

    Jibu

    Simba tupo vizuri yanga msubiri kichapo

    Jibu

    Kumbe simba waoga wameshindwa kushangilia kisa yanga Wana wasi wasi ya kuchezea kichapo jpili

    Jibu

    pole yao wapunguze kiranga.

    Jibu

    Simba ndio mpango mzima kesho#Meridianbettz

    Jibu

    Kocha anawakinga wachezaji wake na corona

    Jibu

    Haha ha haa simba toeni sababu zenu sio kisa yanga msishangilie au mganga wenu ameshaona kuwa mtafungwa achane uoga au mtoe sababu zenu mchezo kesho tusibirie nani anashinda sio mtoe lawama kisa yanga mtachekwa .

    Jibu

    Simba mabigwa

    Jibu

    Simba mko vizuri sana

    Jibu

    Kuna nn tena huko msimbazi

    Jibu

    Tatizo wana msimbazi ni waoga sana ishu ya jpili inawatia kimue mue

    Jibu

    Mna mbwe mbwe sana mbio za sakafuni sikuzote zinaishia ukingoni

    Jibu

    🤣🤣🤣Simba washaanza ona sintofahamu mapema

    Jibu

    Ahahhaaaaaa….hawoookkkkk

    Jibu

    Safi sana Simba ila lazima viongozi wawe na mawasiliano ili kuepuka kutokuelewana mbele za watu .

    Jibu

    Simba wapo vzuri msimu huu

    Jibu

    Mechi za watani wa jadi zinakuwa na mambo mengi sana hasa nchi zetu za kiafrika

    Jibu

    SIMBA soka la bongo wametawala

    Jibu

    THIS IS SIMBA

    Jibu

    Simba damuni

    Jibu

    Matokeo huwanjani

    Jibu

    Wasubiri dabi ipite ndo washerehekee

    Jibu

    Ngoja tuone matokeo uwanjani

    Jibu

    Simbaaa

    Jibu

    Hatariii

    Jibu

    Wasi wasi wao tuu

    Jibu

    Simba lazma wawe na hofu ukiangalia Kwanza wao muda huu wanafurahia ubingwa ila upande wa yanga wanapiga tiz wawe fit kwa mwenye akil ataelewe hiyo siku ikifika Simba kama atachomoka lazam kocha wao awe na hofu kubwa awez kuwa na aman

    Jibu

    Duuh hatari sana.

    Jibu

    kocha anahofu sana kwa sababu mechi ya simba na yanga ni ngumu sana, kwa upande wake endapo simba akifungwa lawama zote zitakua upande wa kocha

    Jibu

    Mh awa nao

    Jibu

    Hakukuwa na mawasiliano mazuri kabla , nadhani Kocha hakufanya vyema#meridianbettz

    Jibu

    Nomaa sanaa

    Jibu

    Simba wanatia sana raha#Meridianbettz

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.