Morison ni Mchezaji Halali wa Yanga na Ana Mkataba - Hersi Said

Klabu ya Yanga kupitia Kampuni ya GSM imemaliza utata sakata la kiungo wa timu hiyo, Bernard Morrison kwamba tayari ana mkataba wa miaka miwili na timu hiyo. Kauli hiyo imetolewa siku moja baada ya kiungo huyo kusikika kwenye vyombo vya habari akieleza kwamba kwa sasa yupo njia panda kufuatia kula dola 5,000 kutoka Simba, ambayo alipewa na wakala wake na ndio maana hakusafiri na timu kwenda Shinyanga.

Akizungumza Dar es Salaam kwenye kituo kimoja cha radio, Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Kampuni ya GSM , Hersi Said alisema anachojua mchezaji huyo ni mali hali ya Yanga, kwani bado ana mkataba wa miaka miwili ya kuendelea kuitumikia timu hiyo.

“Ninachofahamu ni mchezaji halali wa Yanga, mkataba wake wa awali wa miezi sita bado mwezi mmoja unaisha tarehe 14 Julai lakini kutokana ubora wake, tulimsainisha mkataba mpya wa miaka miwili, ambao utaanza Julai 15 na utaisha mwaka 2022,” alisema Said.

Alisema baada ya kusikia sauti ya mchezaji huyo ambaye kwa sasa hajulikani halipo, uongozi wa Yanga una njia sahihi ya kupelekea malalamiko kwenye idara husika na kuona jambo linashughulikiwa kwa haraka. Said alisema kama kuna mtu au timu inamhitaji mchezaji huyo wanapaswa kupita njia sahihi, huku akieleza sababu ya Morissoni kushindwa kusafiri na kikosi hicho kwenda Shinyanga halihusiani na masuala ya mkataba.

Morrison alieleza kwamba wakala wake alipokea dola 10,000 kutoka kwa kiongozi wa Simba, ambaye anatamani ajiunge na kikosi hicho, ambapo nusu ya fedha hiyo alipewa mchezaji huyo na nyingine amechukua wakala ili kujiunga na Wekundu hao wa Msimbazi mkataba utakapomalizika.

45 Komentara

    Ni vizuri abakie hapo yanga

    Jibu

    Bernard Morison nimchezaji mzuri na kila mtanzania na asiye mtanzania hanakili juu ya uwezo wake Ila yanga wasijisahau sababu uwezo wa Morison unaonekana uwanjan ndio maana simba wanamnyemelea mchezaji huyo hata alikuwa na jeuri na kibuli cha kutosha kutokusafiri na timu shinyanga

    Jibu

    Morrison anataka kuzingua

    Jibu

    dah mpira wa kibongo kwel jau yan mchezaj wakimchoka yanga anachukuliwa na simba na akichoka na yanga anachukuliwa na yanga ndo nn sas kwa hali hii sidhan kama sika la bongo litasonga

    Jibu

    Duuu hii nayo habari ngenii kwa kwelii

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Morrison kukijua kiswahili kidogo tu ameanza kusumbua!

    Jibu

    Maamuzi hayo tumuachie mwenyewe#meridianbettz

    Jibu

    uyu Morris sidhan kama yupo sawa anapokeaje ela wakati hajamilizana na yanga bado…?

    Jibu

    Aache kuzingua atulie tu

    Jibu

    Hili la Morrison linachafua hadhi ya Simba kwamba wanashindwa kufuata kanuni na taratibu za kusajiri mchezaji na Viongozi wa Yanga wanapaswa kuongelea hili sio wafadhili GSM kufanya kila kitu!#meridianbettz

    Jibu

    Mali ya yanga wengine watulie

    Jibu

    Morison akiama kwenda simba yanga kutakuwa hamna kitu tena maana bado wanamuhitaji

    Jibu

    Huyu ndiye Bernad Marison hanaga masiahara

    Jibu

    Namkubali Sana

    Jibu

    Daaaah hatari

    Jibu

    Mpira wa Bongo bhana, hizi zinaitwa figisu figisu.

    Jibu

    Huu ni utata ambao ulikuwa unahitaji ukataji wa fitina ili ifahamike maana vyombo vya habari vilikuwa vinaongea mengi

    Jibu

    Bora amesaini kwenye timu ambayo Ndio iliyomleta Tanzania

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Mbona anazingua huyo morson,mala simba mala yanga mbona haeleweki

    Jibu

    Simuelewagi

    Jibu

    Maoni:simba wanatamaa wanamtaka Bernad marison wameona yanga wanafaidi tena

    Jibu

    Morrison baba lao

    Jibu

    Habar njema kwetu wanayanga

    Jibu

    Yuko vizuri sana

    Jibu

    Morison ni 🔥

    Jibu

    Safi sana meridian kwa makala nzuri#meridianbettz

    Jibu

    Kiungo fundi

    Jibu

    duh sio mchezo, simba vipaji vinatosha tayar hatumuitaji huyo jamaa

    Jibu

    Safi sana Morison utaweza kuipeleka yanga mbele siku za mbeleni

    Jibu

    Tatizo tamaa

    Jibu

    Asante kwa makala#meridianbettz

    Jibu

    Morrison fundiiiii wa mpira bongo

    Jibu

    Morison ni mchezaji mzuri kila mmoja analifaham ilo Kama ayuko tayari kuitumikia club hiyo inapaswa afuate taratibu na Sheria za mkataba wake ukimruhusu afanye maamuzi sahihi na clubu anayo itaka kwa sasa

    Jibu

    Pila la bongo bhana eti mchezaji anaigomea club eti na anazima simu kuwa haendi kucheza match

    Jibu

    Yanga wajipange tu wamtafute mchezaji mkali kuliko yeye ili maringo yamuishe

    Jibu

    Morison nakukubali sana ila unataka kuleta miyeyusho sasa kama unataka kusepa fuata kanuni na utaratibu wamkataba wako kama unakuruhusu sawa

    Jibu

    Hongera

    Jibu

    Abaki tu na yanga yake#Meridianbettz

    Jibu

    Yanga wanapaswa kuongelea hili sio wafadhili GSM kufanya kila kitu!#meridianbett

    Jibu

    Abaki tu yanga #meridianbettz

    Jibu

    Yupo vizuri anajua Morison ila amalizie mkataba wake angalie ustarabu mwingine

    Jibu

    Morrison mzunguaji huyo

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.