Muhammad Alli na Joe Frazier mwaka 1975 Lazima Bingwa Apatikane

Maumivu yaliyoje kukosa nafasi ya kutazama pambano la mwisho kati ya Mohammed Alli na Joe Frazier. Lilikuwa Pambano la kusimamisha dunia, pambano la kuzima jua na pambano la kutuliza bahari.

Muhammad Alli na Joe Frazier walikuwa wanakutana kwa mara ya tatu. Frazier alishinda pambano la kwanza, Alli alishinda la pili, hili la tatu lilikuwa la kumaliza ubishi wa nani mbabe. Mara hii likifanyika mji wa Manilla, Ufilipino.

Zilikuwa zimebaki dakika 15 ifike saa tano asubuhi kengele ya kuashiria pambano lilianze ilipopigwa ndani ya Araneta Queizone. Muhammad Alli kama kawaida yake alianza vurugu zake mapema sana, akimtupia Frazier matusi kabla hata hajaanza kurusha ngumi. Joe alimchekea tu na kumwambia “Huna kitu leo”.

Alli alishinda round ya kwanza na ya pili. Akaanza kwa kasi round ya tatu akiendelea kumtukana Joe na kumuambia maneno ya kejeli kama “nipige kwa nguvu nyani wewe.. tatizo ngumi zako laini kama za mke wangu. nakuambia ntakuua leo”. Ila ni katika round ya tatu Joe alifanikiwa kuingiza ngumi ya kwanza kwa Alli.

Frazier aliendelea kumuwashia moto Alli katika round tatu zilizofuata. Alli akarejea kutawala round ya saba na ya nane. Katika round ya tisa Alli alikimbilia pembeni na kumuambia ‘corner man’ wake “ndugu yangu nakufa, kweli tena nakufa kabla sijaandika urithi”. Upande mwingine wa ulingo Joe Frazier alikuwa anaugulia maumivu ya uso uliovimba kiasi cha kumziba jicho lake la kushoto.

‘Corner man’ wa Frazier alitupa taulo ulingoni katika round ya 14, japo bondia wake alishinikiza anataka kuendelea. Baada ya pambano Joe Frazier alisema “kweli yule jamaa ni shujaa, nimempiga ngumi zinazoweza kudondosha ukuta, ngumi zinazoweza kumdondosha farasi asinyanyuke tena”.
Alli yeye alisema, “sijawahi kusogelea kifo kama leo, Frazier alikubali yaishe sekunde kadhaa kabla yangu”.

31 Komentara

    Ama kwa hakika lilikiwa ni pambano la haina yake mana kila mmoja halikumbana na kipigo

    Jibu

    Dah mpaka unatamani ungekuwa kwenye nafsi ya corner wa Frazier

    Jibu

    Duuh hii ilikua zaid ya pambano n zaid ya vita maana si kwa matukio hayo ya kustajabisha na ngonjera zote kila mtu akiomba tukio liishe kila mmoja alijiona hafai kwa mwenzie hii kali kuliko

    Jibu

    navuta picha hili pambano lilikuwaje ngoja nikalisake nione

    Jibu

    Kila mmoja alijiona hafai kwa mwenzie

    Jibu

    Duuh hakika pambano ili ni lakibabe

    Jibu

    Duuuh..! Yani mtu unakufa uku unajiona michezo mingine siyo poa

    Jibu

    Kwel huu mchezo sio poa mtu anae cheza mchezo wa ngumi muache ale pesa yake mwenyewe maana sio kwa shuruba hii

    Jibu

    Mapambano ulikuwa wa kipekee sana huu .

    Jibu

    Mapambano ulikuwa watari sana

    Jibu

    Duuuh

    Jibu

    Mbona mambo yalikua makubwa

    Jibu

    Zamani mpambano ulikua wa ukweli sana

    Jibu

    💪pambano la kibabe hakika.

    Jibu

    Ile cku hakika haitoweza sahaulika kwa mashabk..

    Jibu

    Ile siku hakika haitoweza sahaulika kwa mashabik

    Jibu

    Alli Alikuwa bondia hatari sana anapokuwa ukingoni

    Jibu

    Inadaiwa lilikuwa pambano la karne. Walikuwa wakweli kwamba kila mmoja alikuwa mkali#meridianbettz

    Jibu

    Hii siku haitoweza sahaulika kwa mashabki

    Jibu

    Pambano la kufa mtu

    Jibu

    Pambano Kali Sana ili mshindi apatikane

    Jibu

    Hili pambano lilikuwa Kali sana mana hakuna aliye kubali kumpa mwezake ushindi walivumilia mpaka mwalimu wao akarusha taulo chini kuashiria kukatishwa likatishe lakini wao walipigana kiuhakika hili mbambano nilikuwa la kishujaa

    Jibu

    Mmh hatari sana.

    Jibu

    walivumilia mpaka mwalimu wao akarusha taulo chini kuashiria kukatishwa likatishe lakini wao walipigana kiuhakika hili mbambano lilikuwa la kishujaa

    Jibu

    Lilokuwah pambano la kipekeeh hlo

    Jibu

    Aiseee hilo pambanoo lilikuwa fireeee

    Jibu

    Frazier amejiwekea rekodi kubwa sana kwenye ulimwengu wa masumbwi kwa kumtandika mkali wa masumbwi Muhammed Alli

    Jibu

    Duh kwer Ally shujaa

    Jibu

    Ila mwamedi kama mwamedi alitisha sana#Meridianbettz

    Jibu

    Apo mshindi lazma apatikane

    Jibu

    Pambano kal sana hili

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.