Kocha wa klabu ya Manchester United Ralf Rangnick ameionya klabu hiyo kutofanya tena makosa na kusema kuwa haipaswi kufanya tena makosa kwenye dirisha la usajiri ikiwa wanataka kushindana na klabu za Manchester City na Liverpool.
Ralf Rangnick ambaye jioni ya leo anakwenda kucheza na Manchester City kwenye dimba la Etihad kwenye derby ya jiji la Manchester, ambapo Pep Guardiola anahitaji ushindi ili aweze kujihakikishia nafasi ya kwanza kwenye msimamo, wakati Man Utd wapo nafasi ya nne na bado inaonekana kuwa ni ngumu kuweza kuilinda nafasi hiyo.

“Kuwa na mpango wa wazi wa usajiri na kusajiri wachezaji watakao ingia moja kwa moja kwenye mfumo ndicho ambacho klabu zote zimekuwa zikifanya kwa miaka mitano au sita.” Alisema Ralf Rangnick.
“Nikiangalia sera zao {Man City} za usajiri na mafanikio ya usajiri, hawana wachezaji ambao baada ya mwaka au miaka miwili, watu wangesema kuwa haukuwa usajiri mzuri, klabu zote zimekuwa na mafanikio mazuri na hili ndilo ambalo Manchester united inabidi tufanye tena.”
Ndani ya miaka mitano klabu ya manchester imefanya uwekezaji mbaya wa wachezaji kama Romelu Lukaku, Alexis Sanchez, Donny van de Beek na Dan James. Kwa sasa klabu ya Man Utd iko busy kuweza kutafuta kocha atakaye chukua mikoba baada ya muda wa kocha wa muda kuisha.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.


