Tetesi za Soka Barani Ulaya

Tetesi za soka barani Ulaya leo Jumanne Mei 25, 2021 zinasema:-

Tetesi zinasema, Klabu Borussia Dortmund wamemwambia winga wa England Jadon Sancho, 21, kuwa anaweza kuihama klabu hiyo katika katika dirisha la usajili la majira haya ya joto. 

Tetesi za soka.Tetesi zinasema, Meneja wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer ameweka kipaumbele katika kumsajili Sancho baada ya msimu huu kukamilika japo baadhi ya wachezaji wake wanaishawishi klabu hiyo kumsajili mkataba kiungo wa Aston Villa na England Jack Grealish, 25.

Tetesi zinasema, Real Madrid wako tayari kupokea ofa za timu zitakazotaka kuwasajili winga wa Wales Gareth Bale, 31, na kiungo mshambuliaji wa Ubelgiji Eden Hazard, 30.
Tetesi za soka.Tetesi zinasema, Hazard anataka kurejea tena Chelsea, ambako aliondoka na kujiunga na Real mwaka 2019.

Tetesi zinasema, Klabu ya Tottenham ina mpango wa kumuuza kiungo wao mshambuliaji, Dele Alli, 25.

Tetesi zinasema, Dele Alli apigwa marufuku kwa kuonyesha ishara ya kidole cha kati

Tetesi zinasema, Mshambuliaji machachari Luis Suarez anasema ataendelea kubaki na mabingwa wa La Liga msimu huu klabu ya Atletico Madrid, licha ya kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 kutoka Uruguay amekuwa akihusishwa na taarifa za kurejea katika klabu ya Liverpool.

Tetesi zinasema, Klabu ya West Ham ina hofu Manchester United watawazuia kusaini mkataba wa kudumu na winger wa England Jesse Lingard. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, ameivutia timu hiyo ambayo ameichezea kwa mkopo katika msimu huu.
Tetesi za soka.Tetesi zinasema, Juventus wako tayari kumuuza mchezaji wa safu ya kati kutoka Wales Aaron Ramsey mwenye umri wa miaka 30.

Tetesi zinasema, Barcelona wanajiandaa kuanzisha mazungumzo mapya juu ya mkataba na mshambuliaji Mfaransa Ousmane Dembele. Mkataba wa mchezaji huyo wa miaka 24-unaisha katikati ya mwaka 2022.

Tetesi zinasema, Barcelona na Bayern Munich zinajaribu kusaini mkataba na kiungo wa kati wa Liverpool na Uholanzi Georginio Wijnaldum, 30, wenye kipengele huru cha uhamisho.


BONASI YA 50% KILA SIKU KATIKA KASINO ZA EVOPLAY HAPA MERIDIANBET.

Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.

tuchel, Tuchel :Tuna Bahati Tottenham Wametusaidia Kazi., Meridianbet

SOMA ZAIDI

2 Komentara

    Zote Ni bomba

    Jibu

    Ziko poa

    Jibu

Acha ujumbe