Fainali ya Ligi ya Mabingwa – UEFA kuhitimisha msimu wa 2019/20. Ni mtanange wa aina yake utakaowakutanisha miamba ya Ujerumani – Bayern Munich dhidi ya matajiri wa Paris – PSG.
Kiufundi, huu ni mchezo ambao utakuwa wa aina yake. Timu zote 2 zina nafasi ya kumuumiza mwenzake na kuandika historia ya namna yake. PSG wamefika Fainali ya UEFA kwa mara ya kwanza na wanatazamia kubeba kombe hilo kwa mara ya kwanza katika historia ya timu hiyo.
Bayern Munich sio wageni wa Fainali ya Ligi ya Mabingwa, lakini wanataka kuweka rekodi ya kubeba makombe 3 kwa msimu mmoja wakiwa tayari wameshabeba mawili kunako Bundesliga.
Upekee wa Fainali ya UEFA upo kwenye mifumo ya uchezaji wa timu hizi.
Bayern wamekuwa wakitumia sana mfumo wa 4-2-3-1, mfumo ambao umelenga zaidi kushambulia na unawatumia mabeki wake wa pembeni katika kushambulia. Huu ni mfumo ambao umewapatia matokeo mazuri wakiwa hawajapoteza mchezo wowote katika mechi 29.
Mfumo huu ndio uliopeleka vilio Barcelona na Lyon. Hawapotezi nafasi kirahisi na kuwapa shida wapinzani. Uwezo wa wachezaji mmoja mmoja katika kikosi cha Bayern pia ni faida katika mfumo huu. Gnabry, Alphonso Davies, Kimmich, Lewandowski,Muller na Perisic ni kati ya wachezaji muhimu wa Bayern.
Pamoja na ubabe wa Bayern, kama watajisahau sehemu yeyote, Mbappe, Di Maria na Neymar watawaumiza kutokana na uwezo wao wa kukimbia na mipira.
Kwa upande wa PSG, wao wanatumia zaidi mfumo wa 4-3-3 pamoja na uwezo binafsi wa wachezaji wao hasa washambuliaji. Uwezo wa Mbappe akiwa na mpira na kasi aliyonayo ni dhahiri mabeki wa Bayern watakuwa na kazi ya ziada.
Neymar amekuwa akichezewa faulo nyingi kutokana na namna ya uchezaji wake unaotumia ujuzi mwingi na mbio. Kwa namna ya uchezaji wake, timu pinzani nyingi zinakuwa na wakati mgumu kumkaba kwani nafasi ya kupata kadi ya njano au nyekundu ni kubwa.
Di Maria amekuwa akisahaulika mara kadhaa na mabeki wa timu pinzani, lakini mashambulizi ya PSG yanachochewa na uwezo wa winga huyu mwenye spidi na ufundi wa kutumia mipira ya adhabu.
Kwa sababu hizi na nyingine nyingi, ni dhahiri kumtaja bingwa wa mchezo huu ni ngumu lakini ni mchezo utakuaokuwa na magoli kwa timu zote endapo kila timu itatengeneza na kutumia nafasi za magoli.
Drops and Wins!
Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.
Ernest
Ukiangalia vikosi vyote viwili unapata picha ya soka tamu sana na magoli ya kideo siku ya fainali, sio mechi ya kukosa kuangalia
Issa
Tutaona ufundi mwingi kwenye hii mechi lakini mwisho wa siku bayern atabaki na ndoo tu haina ubishi
Neema
Kwelii mechii sio za kitoto hizoo.
JULIANA
Mapema kitaeleweka
Mwanahamisi
Bora kieleweke
Zeiyana
Kwa kuangalia hii gemu hunaona kabic Bayern kesho hawana kazi ngumu kabic ila tusubiri tu kuwapa pongezi PSG kwa kushiriki na sio kua mabingwa si kweli
Nasra
Hatarii hii
Sauda
Mtanange mkali sana
Tatu
Huu mchezo autaji hasira kila kikosi Leo kimejipanga sawasawa PSG atoweza kumuachia bayern
Sauda
Mechi kali sana
Dorophina
Mechi sio ya kukosa kabisa nataka niwaone watoto wa matajiri PSG watakavyo fanya yao
Sylvester
Nimewakataa sana Bayern kwa muda ila katika fainali naimani atamfunga PSG na kunyakua taji ingawa itakua mechi ngumu sana ya kukata na mundu si ya kukosa kuiangalia
Mwajumah
Kweli mechi hizi sio za kitoto#Meridianbettz
magdalena
kabisa ni mechi ya kipekee inayosubiriwa kwa hamu kubwa na tulio wengi
Khadija
Hatari hii#meridianbettz
Lydia Emmanuel Magoti
Hatarii bonge lamechi apatoshi hio mtanange nyavu kutikiswa kila goli lamtu lazima kushambuliwa
Adelta
Hii mechi Kali sana tunasubiri kwa hamu tuone matokeo@meridianbettz
Fatina mfingi
Huu mtanange mzito Kila timu ipo vizur ukiangalia bayern wapo vizur psg nao wamoto kwaiy hii mechi itakuwa nzur San Ila wenyew wanakwambia mpira dakika 90 ngoj tuone!!
Caroline
Tunasubiri fainali kwa hamu
Adelta
Hii mechi Kali sana tunasubiri kwa hamu tuone matokeo @meridianbettz
Amiri Kayera
Vikosi vyote bola
Janeflora malisa
Mambo mazur
aisha
Tunasubili kuiona fainali kwa hamu sana maana patakua hapatoshi
Sadick
Wabashiri kote duniani tunaipa nafasi Bayern lakini ktk mchezo lolote linaweza kutokea kwa anayeamuka vizuri hushinda na anayeamuka vibaya hupoteza. Pamoja na ufundi wa kocha lakini wakati fulani ni bahati ndi huchukua nafasi zaidi#meridianbettz
Hope mwaikuka
Hii mechi ni balaa maana wote wako vzur
Povel
Don’t miss
Rehema
Safi
lombo
bayern piga hao kama kawa ida yetu LIKE FATHER LIKE SON baba kafa 8 bado mtoto
Gabriel
Hii mech n ngumu sana na kutokana na mifumo yao ya uchezaji wote n wa ushambuliaji hapa ninamaana mechi itakuwa ya kibabe balaa
Devotha
Hii mechi itakua inamagoli mengi maana kila timu naona safu ya ushambuliaji iko vizuri kuzidi safu ya ulinzi
Rose kapinga
Nyasi zitawaka moto sio kwa kandanda iloooo!!!
Shafii
Hii fainali ni ya mvuto Sana maana inawakutanisha mabingwa wa ligi mbili tofauti.
Salma ngende
Vikosi vyote viko vizuri
Omary lukumbi
Hii hatumwi mtu dukan
David Pere
Kwa upande wa PSG, wao wanatumia zaidi mfumo wa 4-3-3 pamoja na uwezo binafsi wa wachezaji wao hasa washambuliaji. Uwezo wa Mbappe akiwa na mpira na kasi aliyonayo ni dhahiri mabeki wa Bayern watakuwa na kazi ya ziada.
Edgar
Kabisa Ni mechi ya kibabe
Ester jackson
Safu zote ziko vizuri pamoja na wachezaji wao hapa haifahamiki nani ataondoka na ubigwa huo mana wrote wanauwezo Wa juu sana hivyo tunasubiri kuona dk 90
farida ahmadi
Hakika mtanange mkali Sana patakuwa hapatoshi
Samiah
Safi
Furahav
Utakua mchezo wa kusisimua.
Sabrina
Itakua balaa
Latifa juma mohamed
Itakua hatari.
warda
Kwa kweli ilikuwa Ya kipekee#Meridianbettz