Zlatan Ibrahimovic Anaamini Yeye ni Bora Kuliko Ronaldo na Messi

Ukweli haujui uongo ila uongo siku zote unaujua ukweli, ili uwe mkweli unahitaji tu kuwa mkweli, lakini ili uwe muongo lazima uishi katika kivuli cha ukweli siku zote. Ibrahimovic amechagua kuishi katika kivuli cha ukweli, moyo wake uliojaa uongo umeulevya mpaka ubongo wake, kikombe cha mahaba juu ya kipaji chake kimemfanya kuwa mtumwa wa nafsi yake.

Nafsi yake haishi tena ile kweli anayopaswa kuishi, inamfanya kujiona ndiye mchezaji bora kuwahi kutokea duniani, ameamua kuwa kinyume na dunia nzima ya soka. Kibaya anaona dunia ndiyo inamkosea heshima sana, heshima wanazopewa Lionel messi na Cristiano yeye alistahili kupewa zaidi yao, hatazami makubwa waliyofanya.

Akiwa Barcelona Zlatan Ibrahimovic aliwaita Messi, Iniesta na Xavi kuwa ni watoto wa shule wanaopendelewa na mwalimu wao, kipindi hicho akiwa ni Pep Guardiola, hakuona sababu ya wao kuonekana bora wakati yeye akiwepo.

Kwa Zlatan anaanza Zlatan ndo wengine wanafuata, Pep Guardiola hakulijua hili mpaka alipoambiwa huwezi kumuweka nje mungu wa mpira kwa ajili tu ya genius messi. Akaondoka zake Nou Camp, moyoni akiamini Lionel Messi hakustahili kuonekana bora zaidi yake ila akilini akauficha uwezo wa kufunga wa Lionel Messi.

Kwa Cristiano Ronaldo, Zlatan Ibrahimovic atakwambia Ronaldo anayemjua yeye vizuri ni yule Ronaldo de lima wa Brazil, hamfahamu mwingine, inawezekana ikawa sahihi kwake. Lakini uongo siku zote unatafuta njia zake kuficha ukweli, atakwambia tena huyu wa sasa ni zao la mazoezi tu kipaji cha mpira hana, kumbe anamjua Cristiano Ronaldo ni ngumu kuuficha ukweli.

Mazoezi ya mpira ni chakula cha kila mchezaji, mbona wanazidiana ubora sasa, anatuthibitishia maneno ya kuwa uongo una njia fupi. Kwa Zlatan Ibrahimovic pia anamuona Pele kama mtu aliyebebwa na nyakati, kwake hana maajabu yoyote yale, amenda mbali na kusema kama yeye angezaliwa enzi za kina Pele zilizokua hazina VAR angeweza kufunga zaidi ya goli 3000.

39 Komentara

    Hata iweje hawezi kuwafikia hao watu labda wastaafu mpira ndio aweze kusema hivo

    Jibu

    Hana jeuri ya kuwafikia hao labda wastaafu ndio aseme ivo

    Jibu

    Zlatan ukubali ukatae Ronaldo bado yupo juu sana kwako

    Jibu

    Ronald Yuko vizuri sana
    Hana mpinzani

    Jibu

    Ronald ni bonge la mchezaji

    Jibu

    Ni mtazamo wake kama anaona yy ni bora kuliko wao sawa yuko sahihi sio mbaya kujiona bora sifa jipe kwanza mwenyewe na ndo utasifiwa na watu wengine

    Jibu

    Ronald yupo vzr sana#meridianbettz

    Jibu

    Ni mtazamo wake so m n nan mpaka nipinge

    Jibu

    Uwo ni mtazamo wake labda kutokana amecheza timu kubwa zote za ulaya

    Jibu

    Huu ni ujasiri wake tu ukweli tunaujua sisi mashabiki ila kwake ni Sawa kabisa haha ha ha

    Jibu

    Zlatan kacheza team kubwa nyingi Ulaya ila kaziletea mafanikio gani?labda bora kwa kalate

    Jibu

    Ronaldo atabaki kuwa Ronaldo mkali wao

    Jibu

    Ayo ni mawazo yake lkn Ibrahimovick yeye sio Bora kuliko Ronald km ni ivy mbn hana ata tuzo moja

    Jibu

    Zlatan Ibrahimovic atasubiri sana kwa hao wamba wawili..

    Jibu

    kweli ni mchezaji mzuri lakini umfikii ronaldo na messi

    Jibu

    Ronaldo yuko vizur sana

    Jibu

    Ronaldo hana mpinzani

    Jibu

    Huo ni mtazamo wke tyuu tena wa kichuki kabsa uwezi jiona bora kwa wenzio ikiwa wanaokuona ukicheza hawaoni ubora wako Zlatan ni mzuri ila kiwango chake sio sawa na Ronald na Messi

    Jibu

    Messi & Ronaldo wachezaji wa sayari nyingine#

    Jibu

    Kuna vitu vichache tuu Kadabra amevikosa na kumfanya azidiwe na Messi na Ronaldo lakini kiukweli huyu jamaa ni hatari sana

    Jibu

    Jamaa ana majidai mengi sana, siku zote anajiona bora kuliko wote. Hata hivyo ni mchezaji mzuri#meridianbettz

    Jibu

    Ronaldo mtu mmbaya sanaaa

    Jibu

    Ronaldn ni mchezaji mzuri

    Jibu

    Rinaldo na Messi ni wachezaji hatari sana mtu yoyote asijifananishe na watu hao

    Jibu

    Ingekua bongo tungesema anatafuta kiki, lakini yeye huko aliko anatafuta nini? anajua fika hiki ni kipindi cha ronaldo na mess!!! naona amesahaulika anataka kukumbusha watu kua na yeye yupo.

    Jibu

    Kila 1 ana mtazamo wake na jinsi anavyojiamini

    Jibu

    labda bora wa taekwando mpira atuache tu

    Jibu

    Kila mtu hanajivunia alicho nacho messi anauchezaji wake lonaldo hanauchezaji wake na yeye anajivunia alichokua nacho

    Jibu

    Nimtazamo wake labda amecheza timu kubwa zote za ulaya

    Jibu

    Akiwa Barcelona Zlatan Ibrahimovic aliwaita Messi, Iniesta na Xavi kuwa ni watoto wa shule wanaopendelewa na mwalimu wao, kipindi hicho akiwa ni Pep Guardiola, hakuona sababu ya wao kuonekana bora wakati yeye akiwepo.#meridian

    Jibu

    Ibrahimovic hampati ronaldo

    Jibu

    aache ndoto zake za mchana labda ajilinganishe na MESS na sio CR7 zile levo nyingne

    Jibu

    Ni Bora Ila hawez kuwah Bora kuwazid Messi na Ronaldo thnks meridian bet tz kwa update

    Jibu

    Ni mtazamo wake yeye

    Jibu

    Hakuna kitu kivuzr kwenye mapambano Kam kujiamin silaha ya Kwanza kweny kupambana ni kujiamin

    Jibu

    Ila messi na Ronaldo wanauwezo Sana.

    Jibu

    Kwa maoni yake na anvyojikubali mwenyewe Ndio maana anasema hivyo

    Jibu

    Zlatan Ibrahimovic huwaga sio shabiki yangu kabisa #Meridianbettz

    Jibu

    Yupo sahihi kwa upande wake

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.