Kanoute Augua Ghafla!

BAADA ya kutoonekana kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Yanga, kiungo wa Simba Sadio Kanoute, Kocha Mkuu wa Simba, Juma Mgunda amesema nyota huyo ni mgonjwa.

Mchezo huo wa ligi ulipigwa jana jumapili kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar ambapo ulimalizika kwa sare ya bao 1-1.

Mabao ya mchezo huo yalifungwa na Augustine Okrah dakika ya huku bao la kusawazisha la Yanga likifungwa na Stephane Aziz Ki dakika ya 45.

Mgunda alisema “Kwanza tunamshukuru Mungu mchezo umemalizika salama, mchezo huu ni mgumu kuliko michezo mingine.

“Kanoute aliumwa ghafla usiku na kupelekea kumuondoa kwenye kikosi kutokana na ugonjwa alioumwa akiwa kambini.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.