James Kotei na Alama Kubwa Aliyoiacha Msimbazi

Ni ngumu kutazama mwisho wa jambo kuliko mwanzo wa jambo, mwisho wa jambo siku zote hubeba kumbukumbu zisizofutika baina ya pande mbili, haswa zikiwa ni kumbukumbu zilizojaa upendo unaoishi moyoni.

Kumbukumbu kumhusu kiungo James Kotei bado zinaishi ndani ya wanasimba, zimegoma kufutika kirahisi haswa wakitazama mwisho wao ulivyokuwa mzuri. Mwisho wa James Kotei ndani ya Simba ulijaa machozi yenye furaha ndani yake, hakuna aliyetamani yaishe, kila shabiki alitamani kufunga mlango wa Kotei kuondoka Tanzania.

Simba yenye miguu ya James Kotei ilikua salama salimini, alijua namna kiungo wa kati anatakiwa kuwa, pindi timu ikiwa haina mpira, ubongo wake ulisoma movement za wapinzani na miguu yake ikapokea maelekezo sahihi ya kupokonya mpira vyema.

Sura ya tabasamu ya Jonas Mkude pale katikati ya uwanja sababu yake kubwa ilikua katika miguu ya James Kotei, maana alimhakikishia pasi pindi atapohitaji kuzipeleka mbele na muhimu zaidi usalama wa timu pindi atapopanda juu kupiga mashuti. Mwalimu Patrick Aussems alikua na uhakika na kile alichokuwa anakifanya sana James Kotei hadi akafikia kuwaruhusu wakina Emmanuel Okwi kuwa free muda wote kuchezea mpira, ni miguu ya Kotei iliyofanyika kafara ili tu timu icheze vyema.

Viungo wa timu pinzani walimchukia pale alipokuwa anakaba, lakini walimpenda pale walipokuwa wanampiga rafu, alikua ananyanyuka taratibu anafurahi, ilikua ni nadra sana kuiona sura ya Kotei ikiwa na hasira.

Akitoka nje ya uwanja anavaa jezi ya taifa stars anapiga selfie, tunamuona ni mmoja wetu, alijua kutufurahisha na tukafurahi kumuona akifurahi. Katikati ya furaha ghalfa James Kotei akatangaza kujiunga na Kaizer Chief, iliwastua wengi sana, ni ngumu sana kupokea mkono wa kwaheri katikati ya furaha ni ngumu sana.

James Kotei

Ingawa machozi yanawahi kukauka lakini macho siku zote hubaki kuwa na majonzi bado majonzi ya kumbukumbu ya James Kotei yanaishi katikati ya wanasimba. Ukitaja jina lake picha inayokuja ni kiungo aliyejua nini Simba inataka katikati ya uwanja, atabakia kukumbukwa kwa sababu kwa heri yake alitoa katika ya upendo na furaha, atabaki James Kotei atabaki James mwana wa Kotei.

42 Komentara

    James kotei alikuwa na mchango mkubwa katika game

    Jibu

    Lazima akumbukwe kotei alikuwa kiungo muhimu sana kwenye klabu

    Jibu

    Hakika wekundu wa msimbazi bado tunamkumbuka sana james.hatutaweza kumsahau kamwe

    Jibu

    Poleni sana wanasimba kwa kubaki na kumbukumbu

    Jibu

    Kumbe aliwapa kumbukumbu nzuri wana simba

    Jibu

    Simba walijawa machozi yenye furaha ndani yake, hakuna aliyetamani yaishe, kila shabiki alitamani kufunga mlango wa Kotei kuondoka Tanzania tunamkumbuka sana shujaa wa simba

    Jibu

    Lazima akumbukwe alikua mchezaji mzuri Sana

    Jibu

    Upendo mkubwa na kujituma kwake kutawafanya wana simba kutokumsahau kirahisii.JAMES KOTEI atabaki james mwana wa kotei jembeee

    Jibu

    James aliwapa kumbukumbu mzuri sn kwenye gemu

    Jibu

    Jemes aliwapa kumbukumbu

    Jibu

    hakuna aliyetamani yaishe, kila shabiki alitamani kufunga mlango wa Kotei kuondoka Tanzania tunamkumbuka sana shujaa wa simba

    Jibu

    Alkua vizur sana enz hzo

    Jibu

    Kotei ni mchezaji mahiri sana na simba hawakukosea kumsajili

    Jibu

    James koteo yuko vizuri namkubali sana

    Jibu

    Kaizer Chief ni club kubwa sana tumtakie kheri kwenye changamoto yake hiyo mpya ya kisoka

    Jibu

    James Kotei atakumbukwa daima

    Jibu

    James kotei ni kumbukumbu kwa sababu alifanya vizuri sana na alikuwa ndo kila kitu msimbazi ,anafaa kuigwa na wachezaji wengine wa timu mbalimbali.

    Jibu

    James Kotei ukitaja jina lake picha inayokuja ni kiungo wenye kujua nini afanye katikat ya uwanja hakika wana simba tulijivunia nyakay ulizokiwepo simba

    Jibu

    Mmoja wa kiungo Bora wakabaji
    Waliocheza Simba sc kwa mafanikio#meridianbettz

    Jibu

    Ahsante kwa habari

    Jibu

    Kafanya vizur sana pale simba

    Jibu

    Kotei anajuwa sanaaa

    Jibu

    James Kotei bado ana nafasi kucheza tena Simba#meridianbettz

    Jibu

    Makala nzur. Meridian

    Jibu

    Kotei anajua sana

    Jibu

    Hii habari imenifurahisha sana,sababu umeniletea mchezaji ambaye nampenda sana mana anakaba hadi kivuli.

    Jibu

    James kotei Yuko vizuri

    Jibu

    Simba awatasahau hii kitu

    Jibu

    Kotei alikuwa mchezaji mzuri Sana kwenye krabu yamsimbasi kwai hawata msau nawatazi kumzungumzia mchezaji huyo anajua James kotei

    Jibu

    James kotei bado tunamkumbuka wana simba

    Jibu

    Kumbukumbu kumhusu kiungo James Kotei bado zinaishi ndani ya wanasimba, zimegoma kufutika kirahisi haswa wakitazama mwisho wao ulivyokuwa mzuri #meridian

    Jibu

    James kotei yuko vizuri Sana

    Jibu

    James Kotei we miss u

    Jibu

    Nimchezaji mzuri aliecheza simba kwa mafanikio

    Jibu

    zilipendwa

    Jibu

    Ni mmoja Kati ya kiungo Bora wa kimataifa kuwah kutokeah mitaaa ya msimbazi thnks meridian kwa update

    Jibu

    Simba walipata mtu ambae ewasaidia sana

    Jibu

    Jamaa fundi

    Jibu

    Kotei mtu hatari sana Yani sijui kwanini Simba wamemwachia aondoke

    Jibu

    Kotei mnyama #Meridianbettz

    Jibu

    Kotei alikuwa kinara mzuri alokubalika kwa kila mtu

    Jibu

    Alikuwa mzur

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.