Anthony Joshua 90% ni Mnaijeria.

Joshua ana asili ya Nigeria na Wanigeria wanajivunia nyota huyo, kwani mama yake ni raia wa nchi hiyo. Pia, baba yake ana asili ya Nigeria na Ireland.

Kuthibitisha mapenzi yake kwa Afrika, bondia huyo amechora ‘tattoo’ ya ramani ya bara hilo kwenye mkono wake wa kulia. Alikulia Nigeria kabla ya kuhamia England alipokuwa na umri wa miaka saba.

Joshua alianza masumbwi mwaka 2007 akiwa na umri wa miaka 18. Aliyemvutia katika mchezo huo hatari ni binamu yake aitwaye Ben Ileyemi.

Anthony Joshua 90% ni Mnaijeria.
Bondia Anthony Joshua.

Miaka mitano baadaye, ndipo aliposhinda medali ya dhahabu katika michuano ya Olimpiki iliyofanyika jijini London, baada ya kumdunda aliyekuwa bingwa mtetezi, Roberto Cammarelle wa Italia.

Dawa za kulevya zilikaribia kumaliza maisha yake ya masumbwi na hiyo ilikuwa mwaka 2011. Alikutwa na dawa hizo aina ya cannabis, lakini alinusurika kifungo cha gerezani. Hata hivyo, alikumbana na hukumu ya kufanya kazi za jamii kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Anamkubali Barack Obama ile mbaya. Joshua amekuwa hafichi mapenzi yake kwa Rais Mstaafu huyo wa Marekani. Akihojiwa na kipindi kimoja cha televisheni, alisema anatamani siku moja angekaa meza moja na Obama.

Anthony Joshua 90% ni Mnaijeria.

Miaka mingi iliyopita, Klitschko aliwahi kumtabiria Joshua kuwa ndiye atakayekuja kutawala ulimwengu wa masumbwi na hicho ndicho kinachotokea sasa. “Hatima ya uzito wa juu wa mchezo wa ndondi iko chini ya Joshua.

“Sijawahi kuona bondia mkubwa, mwepesi na mwenye kipaji kama Anthony na kama ataendelea hivi, mchezo huo ni wake,” aliwahi kusema Klitschko.

Alipokuwa mdogo, Joshua alimpenda mwanamuziki 50 Cent, hasa albamu yake ya ‘Get Rich or Die Tryin’. Alidai kuwa mara nyingi alikuwa na CD ya albamu hiyo na alikuwa akiisikiliza mara kwa mara akiwa na washikaji zake.

Kabla ya kuanza rasmi ngumi za kulipwa, Joshua alikuwa amepigana mapambano 43 ya ridhaa, ambapo alipigwa mara tatu pekee. Lakini pia, kabla ya mwasumbwi alikuwa akifanya kazi za kubeba matofali katika shughuli za ujenzi.


Ondoka na Mkwanja Kwenye Tsh. 160,000,000

Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu.

Soma Zaid

24 Komentara

    Nyumbani ni nyumbani anajivunia kuwa muafrika

    Jibu

    AFRICAN STAND up together 💪💪💪💪💪

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Bondia mkubwa Sana Kwa sasa duniani

    Jibu

    Huyu jamaa sasa ni.bondia wa dunia

    Jibu

    Joshua ni bondia alieweka rekod nzur

    Jibu

    Africa inavipaji vingi sana pongezi kwake

    Jibu

    kijana ana nyota kali sana uyu

    Jibu

    Goodnews

    Jibu

    Madawa ya kulevya yamewasili sana vijana ndoto zao wengi zimepotea

    Jibu

    Kumbe ni mnigeria.sikuwahi kujuaa

    Jibu

    Huyo ni bondia mwenye lekodi zake kafanya mahajabu mengi mno kwenye mapambano yake

    Jibu

    Joshua ni bondia nzuri ila slialikiwa na madawa ya kulevya

    Jibu

    Dogo huwa namkubali sana

    Jibu

    Joshua ngum jiwe

    Jibu

    Dogo anajiamini sana

    Jibu

    Anajiamini sana huyo dogo

    Jibu

    Gud news

    Jibu

    Joshua namkubal sana

    Jibu

    Joshua ni bondia alieweka rekod

    Jibu

    bondia mkubwa sana kwa ss

    Jibu

    Anajivunia asili yake

    Jibu

    Namkubaligi sana uyu dogo

    Jibu

    Hard work always pays

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.