Lionel Messi tayari ana mengi ya kuonyesha kwa kazi yake. Ameshinda Ballon d’Or mara sita zaidi ya binadamu mwingine yeyote – mataji kadhaa ya LaLiga Santander, Pichichi, Copa America, Ligi ya Mabingwa na tuzo zingine nyingi. Sasa, shabiki huko Argentina ameonyesha upendo wake kwa nahodha huyo wa zamani wa Barcelona kwa kujenga Estadio Leo Messi.

Ziko Mendoza, kilomita 1,000 kutoka Rosario kwa kina Messi, ‘uwanja’ huo hauna taa, hakuna uwanja halisi, hauna alama na hauna magoli ya ukubwa wa kanuni. Badala yake, ni uwanja mdogo ulio milimani.
Wazo lilikuwa la mpishi wa Argentina anayeitwa Francisco Javier Guardiola, ambaye hana uhusiano wowote na mkufunzi wa Kikatalani wa Manchester City. Alitaka kutoa heshima kwa Messi kwa kuunda uwanja kwa jina la mchezaji huyo.

Binti wa Francisco, Maca, alituma picha kwenye mitandao ya kijamii ya uwanja huo, akiandika: “Mzee wangu alijijengea uwanja katikati ya milima (Mendoza, Argentina) na kuupa jina la Estadio Leo Messi.
“Ninahitaji uione, tafadhali, ni ndoto ya mzee wangu. Nadhani ni heshima kuliko ile ambayo Barcelona ilimlipa.”
Ibai Llanos, ambaye alikuwa ametambulishwa kwenye tweet hiyo, aliiona na akajibu.
“Mwambie baba yako kwamba nampenda,” Llanos aliandika
“Ilikuwa ni heshima yangu rahisi. Ilikuwa siri, lakini binti yangu aliifanya ijulikane ulimwenguni.”
Haijafahamika ikiwa picha hizo zimeonekana na Messi.
Unawezaje kuikosa hii! Ndani ya kasino za meridianbet kuna mchezo unaoweza kukupa mkwanja mrefu leo hii, Wild Hot 40 ni njia nyingine ya kukufanya milionea, Chagua namba yako na uvune mkwanja.



Sarah
Vizuri
Issa
Saf