Anthony Joshua anapaswa kujifunza sheria za kupigana baadaa ya kupoteza taji la ulimwengu kwa Oleksandr Usyk anasema Michael Hunter.

Bingwa wa Uingereza wa uzito wa juu alibainisha kwamba anaweza kumuongeza Mkufunzi anayeishi Marekani kwenye timu yake baada ya kutembelea viwanja kadhaa vya mazoezi nchini Marekani kufuatia kudundwa na Usyk kwa uamuzi wa alama.
Hunter alipoteza pointi kwa Usyk mwaka wa 2017, ambayo inasalia kuwa doa pekee kwenye rekodi yake, na alitarajia nyota huyo wa pauni kwa pauni kutwaa mataji ya Joshua ya WBA, IBF na WBO.
“Ilienda kama nilivyosema itakwenda,” Hunter aliiambia Sky Sport.
“Anthony Joshua alifanya kile ambacho nilikuwa nikisema mbinu ya mchezo alikuja nayo, mikakati au mwalimu wake nisingeweka yote kwake.
“Kutokana na kujaribu huko kumpiga bondia mzuri haikuwa rahisi kwake, lakini nadhani anaweza kuimarika katika pambano lijalo.”
Joshua anajiandaa kurudiana na Usykmapema mwaka ujao baada ya kupitia kipengele cha marudiano ya haraka.
Lakini Hunter anaamini angeweza kumpa ushauri muhimu kama Joshua angeelekea kwenye uwanja wake wa mazoezi huko Las Vegas.

“Inachekesha, kwa sababu alipokuwa akifanya raundi zake, nilikuwa kama, ‘Laiti angesafiri mahali nilipo sasa hivi.’ Natamani ningekuwa mkufunzi wake,” alisema Hunter.
“Nadhani anazijua sheria lakini nahisi kama hajui namna ya kutumia sheria za upiganaji, tunaweza kumtumia Andre Ward kama mfano siyo mpiganaji mwenye kipaji kikubwa lakini anambinu nzuri ulingoni.
Mkwanja umetema ndani ya kasino za meridianbettz, Mchezo maridhawa wa Aurora Beast Hunter unakupa nafasi sawa ya ushindi leo hii, kila mzunguko una nafasi ya kuibuka mshindi, na mkwanja wako unaupata kila mzunguko utakapo kamilika.


