Timu mbalimbali zinazoshiriki ligi ya NBA zimeanza kujiandaa na msimu mpya 2020/21. Timu ya Houston Rockets ilikuwa na mlinzi wake mahiri – James Harden katika mazoezi.
James Harden anahusishwa na kuondoka kwenye timu hiyo ambapo timu ya Brooklyn Nets na Philadelphia zinatajwa kuwania saini ya mlinzi huyu.
Haijathibitika kama Harden ataondoka au laa lakini mlinzi huyo alijiunga na wachezaji wengine katika mazoezi ya timu hiyo kuelekea kuanza kwa msimu mpya tarehe 22 Disemba, 2020.

Akizungumzia hali ya Harden kikosini hapo, kocha mkuu wa Rockets – Stephen Silas amesema ” tulifanya mazungumzo mazuri na Harden aliporipoti mazoezini. Unaweza kumuuliza yeye kuhusu uwepo wake na vitu kama hivyo, lakini tulikuwa na mazungumzo mazuri.
“Alishiriki vizuri, alikuwa anauliza maswali mazuri na alichangia mambo mengi mazuri , tulikuwa na majadiliano mazuri. Tulizungumzia mpira wa kikapu. Mimi ni kocha wa kikapu na yeye ni mchezaji wa kikapu.
“Kuhusu habari za usajili na vitu kama hivyo, hilo ni jambo lingine mnalopaswa (waandishi wa habari) kumuuliza yeye.”
BURUDIKA NA WANYAMAPORI WAKIIMBA NA KUPIGA VYOMBO VYA MUZIKI!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, furahia mchezo wa Forest Rock. Hapa utaburudika na umahiri wa wanyapori wanaoimba na kutumia vifaa vya muziki wa rock. Burudika huku ukijiwekea nafasi ya kutengeneza pesa ndefu kupitia Meridianbet!!



Caroline
Safi sanaaa
Shakila mrope
Inapendeza san
Rahma
Vizuli
Sarah
Jambo zuri
Dorophina
James yupo vizuri sana
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri sana
Issa
Mtu hatari
Hopemwaikuka
Habar njema hii
Ernest
Habari nzuri kwa The Rockets
Mwanahamisi
Vizuri sana
Janeflora malisa
Safi
Saupha mohamed
Jambo zuriii
samiah
Jambo jema
Tatu
Safi
warda
Huwa namkubali sana James