Mshambuliaji wa Tottenham, Harry Kane amesema ilikuwa ni furaha kubwa kwake kufanya kazi na kocha Jose Mourinho.
Mourinho alitimuliwa kwenye timu hiyo baada ya kupata matokeo mabaya kwenye michezo yake sita mfululizo ya hivi karibuni. Kane kwa sasa ni kinara wa mabao kwenye timu hiyo amesema “Mourinho alikuwa mtu safi sana kwenye timu hiyo.

“Nakushukuru sana bosi kwa kila kitu, ilikuwa jambo zuri sana kuona kuwa tumefanya kazi pamoja.
“Kwa hakika ulikuwa mtu muhimu kwetu, nakutakia kila la kheri kwenye majukumu yako yajayo” aliandika Kane.
Mourinho ametimuliwa siku chache kabla Spurs hawajacheza fainali ya Kombe la Carabao, dhidi ya Manchester City Jumapili ijayo na atalipwa pauni milioni 28, sawa na shilingi bilioni 69 za kitanzania.

Timu hiyo msimu huu imeshindwa kufanya mambo makubwa kwenye ligi ikiwa sasa inashika nafasi ya saba na pointi 50, imeshinda michezo 14 na kupoteza michezo kumi baada ya kucheza michezo 32.
Mbali na Kane, pia staa wa Spurs, Son Heung-min, amesema kuwa anamshukuru sana Mourinho kwa juhudi zote alizofanya kwenye timu hiyo.
Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.



Elika
Shukurani ndio kila kitu
Adelta
Kane amefanya Jambo jema
warda
Wenyewe walikuwa wanapendana
Venerose
Ni Jambo jema kushukuru
aisha
kane amefanya vizuri kwa kutoa shukurani
Magdalena
Mourinho alikuwa na mchango mkubwa Sana ingawa haukuonekana
Sarah
Kane amefanya Jambo zuri
Khadija
Shukurani ndio kila kitu
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri sana
neema hassan
Mourinho kocha mahiri