Bingwa wa kombe la mataifa huru ya Africa Senegal wamepigwa faini na kufungiwa mchezo mmoja ambao itawapasa kucheza bila mashabiki kutokana na utovu wa nidhamu uliofanywa na mashabiki wao kwenye mchezo wa kufuzu kombe la dunia dhidi ya Misri.
Shirikisho hilo la mpira wa miguu duniani FIFA, limeweka katazo la kwa chama cha soka cha Senegal la mchezo mmoja wa ti,u hiyo ya taifa utapaswa kuchezwa pasipo mashabiki na faini ya £143,000 kutokana na kitendo cha mashabiki wao kuwamulika wachezaji wa timu ya taifa Egypt kwenye hatua ya penati.

FIFA walifungua mashataka baada ya shutuma za uvunjifu wa kanuni na ulinzi baada ya mchezo wa pili wa kufuzu, ambapo timu ya nyumbani ilishinda 1-0, kupitia kwa Hamdi Fathi kujifunga na kufanya uwe sawa na kupelekea mchezo kwenda matuta.
Picha zilizochkuliwa kutoka kwenye goli ambalo lilitumika kwa mikwaju ya penati, ilionyesha mianga ya kijani ikiwamuluka wachezaji wa timu ya Misri kila wanapokwenda kupiga mikwaju ya penati.
Salah, Mostafa Mohamed na Ahmed Sayed wote walikosa penati, na Senegal kufanikiwa kujihakikishia nafasi ya kwenda kushiriki michuano ya kombe la dunia nchini Qatar.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


