Joan Laporta Aweka Wazi Mshahara Ambao Mbappe alihitaji!

Raisi wa klabu ya Barcelona Joan Laporta ameweka wazi kiasi cha mshahara ambao nyota wa klabu ya Paris Saint Germain Kylian Mbappe alichohitaji wakati akifanyiwa mahijiano na Cat Radio.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye miaka 23, yupo kwenye mwezi wake wa mwiasho na mabingwa hao wa ligi kuu ya ufaransa, na huku bado kukiwa na kitendawili cha wapi atacheza kwa msimu ujao  huku Real madrid ikiwa ndio klabu iliyo husishwa nae sana kuliko klabu yoyote ile.

Joan Laporta
Joan Laporta

Joan Laporta aliweka wazi kiasi ambacho walipewa ikiwa watahitaji huduma ya mshindi wa kombe la dunia mwaka 2018, Mbappe alihitaji kiasi cha  €50 million kama mshahara wake kwa mwaka, kitu ambacho kisiwengewezekana kutokana na matatizo ya kifedha ambayo klabu hiyo ilikuwa nayo.

“Kylian Mbappe alihitaji kiasi cha €50 million kwa mwaka” alisema Joan Laporta

Kwa sasa Mbappe bado haijajurikana ni wapi atamwaga wino kwa msimu ujao, huku kiwa na taarifa mbili za kila upande PSG wanadai kuwa wana uhakika wa kumbakisha na Real Madrid nao wanadai kuwa tayari washafanya mazungumzo ya awali.


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe