Zorc: Hakuna Mpango wa Kumuachia Haaland.

Michael Zorc ametupilia mbali uvumi unao endelea juu ya staa Erling Haaland kuihama klabu ya Borussia Dortmund na kusema Dortmund ina mpango wa muda mrefu na nyota huyo.

Haaland ameendelea kufurahia maisha yake soka katika ligi ya Bundesliga baada ya kujiunga na Borussia Dortmund akitokea klabu ya Salzburg mwezi Januari mwaka huu na amekuwa anahusishwa na kujiunga na vilabu kama Real Madrid, Manchester United pamoja na Juventus.

Fowadi huyo mwenye umri wa miaka 20 hivi karibuni alishinda tuzo ya Golden Boy 2020, amekuwa mchezaji mwenye kasi zaidi kufunga magoli 15 katika Champions League katika historia ya michuano hiyo baada kufunga magoli mawili kwenye ushindi wa 3-0 dhidi ya Club Brugge siku ya Jumanne.

Haaland ambaye ni raia wa Norway amefunga magoli 10 katika michezo saba ya Bundesliga msimu huu na kufunga magoli 17 katika mashindano yote msimu 2020-21 yakijumuishwa magoli sita katika Champions League.

Ikiwa Haaland anaendelea kuvivutia vilabu mabalimbali vya Ulaya Zorc ameweka bayana kuhusu hatima ya mchezaji huyo akiwa na mkataba wenye thamani ya €75m (£67m) ambao utafanya kazi mpaka mwaka 2022.

“Nafurahi pale ninapoona Haaland anahitajika na timu nyingi hii inamaana kwamba anacheza vizuri wote tunafanya kazi nzuri,” Zorc aliwaambia maripota kuelekea mchezo wa Jumamosi wa Bundesliga dhidi ya Cologne.

“Sitakiwi kusema kitu chochote kwa mameneja wengine, kwa sababu tuna mipango ya muda mrefu na Erling.

Tangu ajiunge na Dortmund mwanzoni mwa 2020, Haaland amefunga magoli 33 katika michezo 31 kwa miamba hiyo ya Ujerumani.

Haaland aweka wavuni magoli 23 katika michezo 22 ya Bundesliga akiwa na Dormund ambao wapo nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama moja katika michezo nane.


USICHELEWE KUKAMATA MKWANJA HUU!

Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.

Meridianbet Tanzania Casino

SOMA ZAIDI

17 Komentara

    Haaland ni wa Dortmund

    Jibu

    Haaland yupo vizuri

    Jibu

    Aende tu

    Jibu

    Hapo tuone anaweza kwenda popote

    Jibu

    Watafanya vizuri kama wakimchukua

    Jibu

    Wamchukuwe tu

    Jibu

    Wakimuachia watakuwa wamepoteza bonge LA mchezaji

    Jibu

    Wamchukua mbn yupo vizuri

    Jibu

    Halaand bonge la mchezaji

    Jibu

    Dortmund hawawezi kumuachia haaland ht iweje

    Jibu

    Hapo afadhal

    Jibu

    watakuwa wamefanya jambo zuri kama watamchukua

    Jibu

    Asepe tu

    Jibu

    Bora wamchukue

    Jibu

    Chombo ya Dortmund hiyo aendi kokote

    Jibu

    Haaland anapasua vichwa vya watu sana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.