KMC Wanazitaka Pointi 3 za Yanga

Kuelekea mchezo wa kesho jumatano dhidi ya Yanga, Kocha Msaidizi wa KMC, Ahmed Ally amesema kuwa mipango yao ni kupata pointi tatu au ikishindikana waipate moja.

Mchezo huo wa ligi kuu unatarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar ambapo Yanga tayari wakiwa wamekusanya pointi 14 na KMC wakiwa nazo 13.

Akizungumzia maandalizi yao, Ahmed amesema wamejiandaa kuelekea kwenye mchezo wa kesho ili kuhakikisha wanatimiza malengo yao.

“Timu ipo vizuri kuelekea kwenye mchezo wa kesho na mipango yetu ni kuhakikisha tunavuna pointi tatu au ikishindikana tupate pointi moja.

“Tunawaheshimu wapinzani wetu wana kikosi kizuri tumewaona kwenye mechi iliyopita hivyo tumeenda mazoezini na kuandaa mipango mipya kwa ajili ya mchezo huo.

“Makosa ambayo yalifanyika kwenye michezo iliyopita tumeyafanyia kazi na kuyamaliza hivyo hayawezi kujitokeza tena na mashabiki wetu tunawaahidi ushindi.”


Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.