Klabu ya Barcelona imeuza sehemu ya umiliki wake kwenye studio yao ili iweze kupata fedha ya mtaji wa kuwasijiri wachezaji wake wapya kwenye kikosi cha timu hiyo kabla ya kuanza kwa ligi kuu nchini Hispania.
Barcelona kutokana na hali ya kiuchimi iliyopo kwenye klabu hiyo na sheria za La liga, miamba hiyo ya Catalunya wasingeweza kusajiri wala kuboresha mikataba ya mchezaji yoyote pasipo kuuza mchezaji au kupunguza mishahara ya wachezaji waliopo.

Barcelona wametangaza kuuza aailimia 24.5 ya umiliki wake kwenye studio ya Barça Studios kwa kampuni ya Orpheus Media kwa kiasi kinachokadiriwa kufikia €100milion.
Barcelona kufanikiwa kuuza sehemu ya mali yake kwenye hatua hii ya nne ya kuinua uchumi wa klabu hiyo kwa kubadilisha mali zake kuwa fedha taslimu, lakini bado haiwapi nguvu ya kuwasajiri wachezaji wake ambao ni Andreas Christensen, Franck Kessié, Robert Lewandowski, Raphinha, Jules Koundé, Sergi Roberto na Ousmane Dembélé.
Ijapokuwa klabu ya Barcelona imefanya maingizo ya pesa nyingi kwenye mauzo ya mali zake, lakini vado watasubiri La Liga waweze kupitia docunents zo ili waweze kijiridhisha ikiwa barca wataweza kuwaongeza wachezaji hao.
Pia Barca wapo kwenye mazungumzo na wachezaji kadhaa ambao ili kuweza kupatana tena kwa ajiri ya kupunguza mishahara yao na waengine wakubali kuvunja mikataba yao au wauzwe ili kuweka sawa payroll yao.
Gerard Piqué na Sergio Busquets ni miongoni mwa wachezaji waliokubali kupunguza mishahara yao, Martin Braithwaite amegoma kupunguza kupunguza mshahara wake, huku Memphis Depay amekuwa akifanya mazungumzo na klabu ya Juventus kkuhamia huko na Frenkie de Jong yeye hana nia ya kutaka kuondoka Camp Nuo.

