Nyota wa muziki wa bongo fleva Raymond Mwa… anatarajiwa kutumbuiza kwenye tamasha la Azam ‘AZAMKA’ litakalofanyika Agosti 14 mwaka huu.
Tamasha hilo litakuwa maalum kwa klabu ya Azam kwa ajili ya kuwatambulisha wachezaji wao huku wakicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Zesco United ya Zambia.

Akizungumzia hilo, ofisa habari wa Azam FC, Thabit Zakaria ‘Zaka zakazi’ amesema kuwa “Mambo yanaenda vizuri na maandalizi yanaendelea kuelekea kwenye tamasha letu.
“Tunatarajia kuwa na msanii atakayetumbuiza ambaye ni Rayvanny katika tamasha letu hilo hivyo tunawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi katika tamasha hilo.
“Tiketi zinapatikana kote kwenye Ice Cream centers na kutakuwa na magari maalumu yakipita kuuza tiketi.”

