Tonombe Apewa Zawadi na Azam

ALIYEKUWA nyota wa Yanga, Mukoko Tonombe ambaye kwa sasa anakipiga kwenye klabu ya TP Mazembe amepewa zawadi ya jezi na Uongozi wa Azam FC.

Tonombe alikitumikia kikosi cha Yanga kwa mafanikio makubwa ambapo aliondoka ndani ya klabu hiyo na kutimkia TP Mazembe kwa makubaliano maalum.

Ofisa Habari wa Azam FC, Thabit Zakaria ‘Zaka zakazi’ ndiye aliyekabidhi jezi hiyo leo wakati Azam wakicheza mchezo huo wa kirafiki dhidi ya TP Mazembe.

Mchezo huo wa kirafiki umepigwa kwenye Uwanja wa Ndola nchini Zambia huku timu hizo zote zikicheza zikitarajia kushiriki michuano ya kimataifa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.