Dana White: Bado Kuna Nafasi ya Khabib Katika UFC

Rais wa UFC Dana White anaamini bado “kuna nafasi ya Khabib Nurmagomedov kureejea tena baada ya kutangaza kustaafu kwenye mchezo huo wa kupigana.
Dana White: Bado Kuna Nafasi ya Khabib Katika UFC
Khabib wakati wa pambano lake la mwisho.

Khabib alishangaza watu wengi baada ya kutangaza kustaafu kufuatia kumpiga Justin Gaethje na kutetea mkanda wa lightweight katika UFC 254 mwaka jana mwezi Oktoba na kufikisha idadi ya ushindi wa 29-0 ingawa alikuwa na umri wa miaka 32 pekee.

White amebainisha kuwa anatumaini la kurejea kwenye mchezo wa UFC, kipindi cha nyuma aliwahi kusema atajaribu kufikia rekodi ya 30-0

Conor McGregor anaendelea kumtolea macho Khabib kwaajili ya pambano, wakati Dustin Poirier ambaye aliwahi kupigana naye na kumshinda kwa TKO kwenye UFC 257 amesema kwamba yeye ni bingwa.

Akiongea kuelekea pambano la UFC 259 White aliwaambia maripota anajiandaa kukutana na Khabib.

“Tutakuwa na chakula cha mchana siku ya Jumamosi au Jumapilitutaongea na kuona nini kinaweza kufanyika,” White alisema.


Ni Muda wa Kuvuna Mkwanja na Jungle Jim and the Lost Sphinx

Hauihitaji kufikira mara mbili ni mchezo gani utakupatia mkwanja ndani ya kasino za Meridianbet. Jiunge sasa ufurahie Jungle Jim and the Lost Sphinx.

  CHEZA HAPA

5 Komentara

    Hii ni bonge la makala

    Jibu

    Vizuri sana

    Jibu

    Itapendeza

    Jibu

    Itakuwa poa

    Jibu

    Ukiwa fiti unarejea tu kusaka pesa

    Jibu

Acha ujumbe