Al Hilal wanatarajia kuwasili nchini leo alhamis kwa ajili ya mchezo huo ambao utapigwa kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar saa 10:00 jioni.

Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe amesema: “Maandalizi yamekamilika kwa asilimia 90 mpaka sasa tunachosubiria ni kuwasili kwa wageni wetu.
“Kocha Nabi amewaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi kwenye Uwanja wa Mkapa siku hiyo kwa ajili ya kuwapa sapoti wachezaji wetu.
“Amesema hili niwafikishie ili waweze kuja kwa wingi kwani wao ni wachezaji wa 12 uwanjani hivyo itaongeza nguvu na morali kwao.”

