Al Hilal Watuma Barua Yanga

UONGOZI wa klabu ya Yanga umefunguka kuwa tayari wageni wao Al Hilal wametuma barua kuwa wanatarajia kufika nchini kesho alhamis kwa ajili ya mchezo wao.

Yanga inapaswa kupata ushindi kwenye mchezo huo wa nyumbani ili kuhakikisha wanatinga katika hatua ya makundi kabla ya mchezo wa marudiano utakaochezwa nchini Sudan.

Akizungumzia hilo, Ofisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe amesema: “Maandalizi yetu kama uongozi yamekamilika na hata yale ya nje ya uwanja.

“Ya nje ya uwanja ni kwa maana kwamba kuwaandalia wageni wetu sehemu ya kufikia kwani tayari wametuma taarifa kuwa wanatarajia kufika Dar kesho alhamis.

“Hatujaingia kwenye hatua ya makundi kwa muda mrefu hivyo mipango yetu ni kuhakikisha tunaiweka rekodi hiyo na wachezaji, benchi la ufundi wanalijua hilo na wameahidi kulitimiza.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.