Gareth Bale anasema amekuwa na furaha tangu aliporudi Tottenham baada ya winga huyo kufunga mabao mawili katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Burnley siku ya Jumapili.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 alipiga bao dakika mbili tu za mchezo kabla ya Harry Kane kuweka jingine dakika ya 15. Baadaye Lucas Moura alifunga goli la tatu muda mfupi kabla ya mapumziko, Bale alimaliza kufunga mapema katika kipindi cha pili alipokutana na pasi kutoka kwa Son Heung-min na kupiga shuti lililomuacha Nick Pope.
Bale alikuwa ameanza mechi mbili tu kati ya nane za Ligi Kuu na alikuwa amefunga mara moja tu kabla ya kuisaidia timu yake kupata ushindi dhidi ya vijana wa Sean Dyche.
“Jambo muhimu zaidi ni kwamba tulijua hatujafanya kazi kubwa na ilikuwa muhimu kurudi kwenye kawida yetu ya kushinda,” aliiambia BBC kwenye Match of the Day.
“Sio tu juu ya kufunga. Ni juu ya kucheza kwetu kwa pande zote na kuisaidia timu. Nimefurahishwa na magoli na assist na chochote ninaweza kufanya kwa timu.
“Nimekuwa na furaha msimu wote. Katika chumba cha kuvaa najisikia raha na nina raha. Nina furaha na nina hakika inaonekana uwanjani.
“Sikukasirika kubadilishwa. Kuna michezo mingi ijayo. Ni muhimu kuendelea kuzitumia vyema dakika kila mchezo.”
BusttheBank ni sloti inayokupa Mkwanja wa kutosha. Ndio, hii ni sloti inayokupa faida ya hadi mara kibao ya dau lako. Ni Meridianbettz pekee utakapoweza kupata burudani hii.
Venerose
Safi sana Bale
warda
Bale karudi tena kwenye form
Neema juma
Katisha sana Bale
Angelina
Bale hana kazi mbovu
Rahma
Bale mtu makin
Adelta
Bale yuko vizuri
Sarah
Bale Yuko vizuri
Issa
Huyu ndio bale
Hopemwaikuka
Namuelewa sana