Lewandowski Awa Gumzo Ulaya

Wawakilishi wa Chelsea wamewasiliana na mabosi wa Bayern Munich ili kuinasa saini ya Robert Lewandowski (32) katika dirisha lijalo la majira ya Kiangazi.

Mbali na kuwasiliana na mabosi wa timu hiyo taarifa zimefichua kwamba tayari Chelsea imeandaa ofa nono kwenye dili hilo kwa ajili ya kumshawishi mkali huyo wa mabao katika Ligi Kuu ya Ujerumani
Lewandowski.Lewandowski anaonekana anataka kuondoka katika dirisha lijalo la usajili ili kutafuta changamoto mpya baada ya kucheza kwa mafanikio makubwa ndani ya Ujerumani.

Bayern yenyewe imeonekana kuwa tayari kumuuza straika huyo, lakini itafanya hivyo kwa timu itakayowasilisha ofa nono zaidi kuliko nyingine. PSG na Barcelona pia zinatajwa kuiwinda vikali saini ya nyota huyo wa kimataifa wa Poland.


UNAWEZA KUWA MILIONEA WAKATI WOWOTE!

Zungusha na ushinde mkwanja wako papo hapo baada ya mzunguko kukamilika. Ni kugusa tu 🤑.

BASHIRI SASA

Acha ujumbe