Rasmi Rudiger ni Mchezaji wa Real Madrid

Antonio Rudiger anasubiri kuanza kazi tu na Real Madrid baada ya uhamisho wake wa bure kwenda kwa mabingwa hao wa Ulaya kuthibitishwa.

Rasmi Rudiger ni Mchezaji wa Real Madrid

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alikataa mkataba mpya nono ya kusalia Chelsea, badala yake akachagua kujiunga na mabingwa wa LaLiga na Champions League kwa mkataba wa miaka minne.

Anaondoka Stamford Bridge baada ya miaka mitano, ambapo alishinda Kombe la FA, Ligi ya Mabingwa,Europa, UEFA Super Cup na FIFA Club World Cup.

Rudiger, ambaye alijiunga kutoka Roma mwaka wa 2017, alisema kwenye Instagram: “Ninajivunia kutangaza kwamba nitajiunga na RealMadrid. Nina furaha kubwa kwa changamoto zote zinazokuja na siwezi kusubiri kucheza michezo yangu ya kwanza kwa klabu hii kubwa.”

Chelsea pia ilithibitisha kuondoka kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani, na kuongeza katika taarifa: “Tunamuaga Antonio Rudiger anapoondoka Stamford Bridge na mkataba wake wa Chelsea ukimalizika, na kuhitimisha miaka yake mitano iliyojaa makombe na klabu yetu.

“Klabu ya Soka ya Chelsea inamshukuru Toni kwa mchango wake katika mafanikio yetu katika kipindi cha miaka mitano iliyopita na inamtakia heri katika maisha yake ya baadaye.”

Real Madrid, ambao waliwaondoa Chelsea kwenye Ligi ya Mabingwa, walisema Rudiger atatambulishwa Juni 20.

Taarifa ya klabu ilisema: “Real Madrid C.F. wamefikia makubaliano ya kumsajili Antonio Rudiger, ambaye anajiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka minne.


 

SHINDA SAMSUNG A32 NA AVIATOR

SHINDA Samsung A32 ukiwa na mchezo wa Aviator kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet! Kwea pipa ukusanye zawadi zako pamoja na ushindi mnono wa mkwanja!

kasa wa njano, Kasa wa Njano Awapa Ubingwa wa CL Liverpool., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

Acha ujumbe