Yanga Kumkosa Lazarious Kambole

KOCHA Mkuu wa Yanga, Nassredine Nabi amefunguka kuwa kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Simba watamkosa straika wao mpya, Lazarious Kambole.

Akizungumzia maandalizi yao, Nabi amesema “Tunashukuru tupo sawa kuelekea kwenye mchezo wetu wa kesho dhidi ya Simba.

“Tumekuwa na maandalizi kwa muda mfupi lakini tumejitahidi kuendana na muda ila kikubwa tumejiandaa vizuri na tunatambua umuhimu wa mchezo huu kwamba unaangaliwa na nchi nyingi Afrika hivyo tuna imani tunaenda kupata matokeo.

“Tutamkosa Kambole kwenye mchezo huo kutokana na kusumbuliwa na majeraha lakini kwa upande wa Jesus Moloko yeye tayari ameanza mazoezi na timu hivyo atakuwa sehemu ya kikosi.

“Kwenye mchezo dhidi ya Vipers tulikuwa hatujajiandaa vizuri kutokana na muda ambao tuliingia kambini tofauti na Vipers lakini nilipata picha halisi ya kikosi changu na haikuwa lazima tupate matokeo katika ule mchezo.”

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.