Kabwili Kuonekana Rwanda

GOLIKIPA wa zamani wa Yanga, Ramadhan Kabwili amesaini mkataba wa kukitumikia kikosi cha Rayon Sports ya Rwanda. 

Kabwili alikitumikia kikosi cha Yanga kwa mafanikio makubwa ambapo alipandishwa kwenye kikosi cha wakubwa akitokea kikosi cha vijana U20.

Kipa huyo anakumbukwa zaidi baada ya kucheza mechi ya dabi ya kariakoo dhidi ya Simba msimu wa 2019/20 ambapo alionyesha kiwango kikubwa licha ya timu hiyo kupoteza kwa bao 1-0.

Bao la mchezo huo lilifungwa na Meddie Kagere ambaye aliunganisha krosi kutoka kwa John Bocco.

Lakini kuanzia msimu wa 2020/21 mpaka kuondoka kwake mambo yalikuwa magumu kwa kipa huyo baada ya maingizo mapya ya makipa ndani ya kikosi cha Yanga ambao ni Metacha Mnata na Faroukh Shikhalo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.